Pages

Tuesday, October 9, 2012

INDONYA NGOMI KUMWANI TWIYANGALILE

Kwa kuwa wameweka kidhungu ngoja tuweke Kiswahili kwa kifupi, TAHADHARI YA MVUA KUBWA NA UPEPO MKALI, KATI YA 8TH OKTOBA NA 11 OKTOBA 2012. MAENEO HUSIKA NI MIKOA YA DAR ES SALAAM, MOROGORO, PWANI, NA VISIWA VYA UNGUJA NA PEMBA. KUNAWEZEKANA KUWEKO NA MVUA KUBWA YA KATI YA 50mm na 100mm KATIKA KIPINDI CHA MASAA 24,

Monday, October 8, 2012

WAZEE WA KIHESA 3- MZEE LOTTI LUPEMBE

-->   Mzee huyu wa kabila la Kibena alikuwa mkulima wa kawaida sehemu za Isimani kama ilivyokuwa kawaida  ya wazee wengi waanzilishi wa Kihesa. Baada ya mavuno mazuri walijenga nyumba zao  Kihesa. Mzee lotti alijizolea umaarufu  Kihesa kwa tabia yake ya kujitolea kupita asubuhi na mapema karibu kila mtaa na kutoa matangazo kwa wananchi , kwa mfano mtoto kapotea, ama kuna msiba umetokea n.k, kutokana na umaarufu huo wa Mzee Lotti, pale kihesa kuna mtaa unaitwa kwa LOTTI LUPEMBE .

Sunday, October 7, 2012

WAZEE WA KIHESA -2-MZEE ISAYA KIGAHE

MFARANYAKI CLUB
Mzee huyu wa kabila la Kibena ambaye mpaka leo yupo pale Kihesa, ni mmoja ya wazee waliofika eneo la Kihesa miaka ya 1940. Ukiachaa mwanae wa kwanza Gerald Isaya Kigahe ambaye amefariki miezi michache iliyopita, Mzee huyu alikuwa na mwanae  aliyeitwa Naftari Isaya Kigahe aliyefariki takribani miongo miwili iliyopita. Naftari  alikuwa JEMBE kwa wana kihesa, huyu bwana ndio mmoja wa wawaanzilishi wa lile eneo la Mkimbizi ki ujenzi na likaitwa kwa Kigahe. Moja ya vitu ambavyo vilimgalimu Naftari kuanza kukaa eneo hili ni kuvamiwa na majambazi na kupigwa risasi, aliuguwa na kupona majeraha na kuendelea na shughuli zake kama kawaida. 
Naftari Kigahe ndiye mwenye watoto akiwemo Rogers, Christina, Ganma na mkewe se Msamba maarufu Mama Kigahe bado yupo, Mkimbizi kwa Kigahe anaendesha biashara zake. Kwa waliosoma shule ya msingi ya Chemchem , miaka hiyo ikiitwa Consolata Primary school watamkumbuka Naftari kuwa alikuwa ndiye alikuwa mpiga ngoma kubwa katika bendi ya shule miaka hiyo. Bendi iliyokuwa chini ya Mwalimu Daudi Luhanga.

MBUNGE WA ZAMANI WA MUFINDI AFARIKI DUNIA

Habari zilizotufikia muda si mrefu ni kuwa Mbunge wa zamani wa  Jimbo la Mufindi  kusini, Mhe.Benito Malangalila amefariki dunia  jana katika hospitali ya wilaya ya Mufindi mjini Mafinga mkoani  Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi Amina.

WAZEE WA KIHESA -1-MZEE PHILIPO SAWANI

Mzee huyu wa kabila la Kikinga ambaye ni mmoja wa waanzilishi wa Kihesa alikuwa mkulima eneo la Ngano Isimani. Huku akiendesha biashara ya duka na bar hapo KIHESA katika nyumba yake ya kisasa kabisa. Wazee matajiri wa mji wa Iringa mfano Mzee Mwaitebele, Mzee Idd Mwangubi, Mzee Zabron Mwanyato pamoja na wafanya kazi maofisa kama Mzee Asam Sajio Kaduma walipenda kunywa kwenye bar ya Mzee Sawani. Lakini pia alipokuwa Mwenyekiti wa Tanganyika African Parents Association (TAPA) wa wilaya na alinunua jengo kwa pesa zake na kulifanya shule ya TAPA ambayo kwa sasa inaitwa Shule ya Msingi Mtwivila. Na mwalimu wa shule hiyo wa kwanza alikuwa Mwalimu Edward Chaula ( Baba Kichupa ) na Joseph Msandi ambao mishahara yao ililipwa na mzee Philipo Sawani. Jully Sawani ni mtoto wa Mzee Sawani ambaye alikuwa diwani wa kwanza Kihesa. Mzee Sawani alikuwa  mtu nadhifu sana akipendelea kuvaa English suit. Ama kwa hakika Mzee Philipo Sawani ana mambo mengi sana aliyochangia kwa Kihesa na maisha ya wengi tukisema tuyaandike yote hapatoshi.

Friday, October 5, 2012

WANAKIHESA WAONGEZEA MAJINA YA WAANZILISHI WA KIHESA

-->

Katika hii orodha ya wazee wa Kihesa waongezwe hawa:

1.   Mzee Mtwivila,
2.     Fabian,
3.    Bibi Semtema,
4.    Mzee Lwaho,
5.     Victo Mwibalama,
6.     Mzee Mwambua (Baba Mussa),
7.     Mzee Ally Ngimba,
8.    Edward Wissa,
9.    Mgeni (Baba Jenifa),
10.                Kavilwa (Mourise),
11.                Msigomba,
12.               Balama (Baba Vero),
13.                Balama (mnyakilabu),
14.                Kibassa (Baba John),
15.               King Miking Kibassa (Babu yangu),
16.                Mzee Ng'owo,
17.                Ngogo (Mwanji),
18.               Tenga's wote (kuanzia Ngimonyi hadi wengine),
19.                Kalinga (Baba Moses),
20.               Nyalusi (Baba Mercy wa Timber),
21.                Mgeni (MZALENDO),
22.               Kigahe,
23.               G.G. Shambe,
24.               John Mbegalo,
25.               Gwegime (watoto wake hadi leo machampion),
26.                Sambala (Baba Marcelino),
27.               Mzee Luhanga (Baba yake Mwanyenza),
28.               Mzee Cheka (Baba ya Cheka Club Semtema),
29.                Mzee Gohage (Babu Fredy),
30.               Mzee James (Baba Baldo),
31.                Mwanzo Mgumu (Chao),
32.                Abel Lulandala (Baba Aidan),
33.                Fivawo,
34.               Mzee Kisonga.
 Pia orodha bado ni ndefu sana TUSAIDIANE KUIBORESHA

ENDELEA KUIJUA HISTORIA YA KIHESA

 WASIFU WA WAZEE WAANZILISHI WA KIHESA

 (1) MZEE JUMBE OMARY  
  Huyu mzee makazi yake ya mwanzo yalikuwa Kigonzile, baadae aliamia Kihesa karibu na mlima lilipo  kanisa la Kilutheli la Kihesa. alichaguliwa kuwa JUMBE,
Kazi yake aliamua kesi mbalimbali na kuwahamisha watu kuja eneo ilipo Kihesa kutoka  milimani, kwa mfano mlima Mafifi.
Kesi zilizo mshinda alizipeleka Kalenga wakati huo ndiko kulikwepo mahakama ya mwanzo. Mwandishi wa habari hii alimuona Mzee JUMBE OMARY mara ya mwisho mwishoni mwa miaka ya 1970. Alikuwa na ngeu usoni ambayo inasemekana  aliwahi kupigana na simba.

(2) AZIZA SEMGENI
 
 Bibi huyu ni mmoja wa waanzilishi wa Kihesa, yeye alikuwa anatibu kwa miti shamba, Eneo lake ndipo palipo jegwa shule ya msingi Kihesa. Wajukuu wa Bibi Aziza ni Mzee Jonas Mgeni ( Baba Zacho) Mzee Lwinusu Mgeni (Baba Riziki)

(3) SEMTEMA KUUKINGA
Mama huyu wa kabila la Kikinga aiifariki miaka michache aliopita ni mmoja wa waanzilishi wa Kihesa na alikuwa anamiliki eneo ambalo mpaka leo maarufu kwa jina la SEMTEMA  karibu kabisa na Chuo Kikuu cha Tumaini

(4) SALUMU SOSOVELE
Huyu mzee kwa waliobahatika kumuona alikuwa pandikizi la mtu. mwenye kuongea kwa tabasamu. Baba yake mzazi ndie aliyemiliki eneo kilipo jegwa Chuo Cha Elimu Kleruu.Na kaburi la baba wa Salum lipo jirani na Kanisa Katoliki Kihesa.

STAT COUNTER