Mzee huyu wa kabila la Kikinga ambaye ni mmoja wa waanzilishi wa Kihesa alikuwa mkulima eneo la Ngano Isimani. Huku akiendesha biashara ya
duka na bar hapo KIHESA katika nyumba yake ya kisasa kabisa. Wazee matajiri wa
mji wa Iringa mfano Mzee Mwaitebele, Mzee Idd Mwangubi, Mzee Zabron Mwanyato
pamoja na wafanya kazi maofisa kama Mzee Asam Sajio Kaduma walipenda kunywa
kwenye bar ya Mzee Sawani. Lakini pia alipokuwa Mwenyekiti wa Tanganyika African Parents Association (TAPA) wa
wilaya na alinunua jengo kwa pesa zake na kulifanya shule ya TAPA ambayo kwa sasa
inaitwa Shule ya Msingi Mtwivila. Na mwalimu wa shule hiyo wa kwanza alikuwa Mwalimu Edward Chaula ( Baba Kichupa ) na Joseph Msandi ambao mishahara yao ililipwa na mzee
Philipo Sawani. Jully Sawani ni mtoto wa Mzee Sawani ambaye alikuwa diwani
wa kwanza Kihesa. Mzee Sawani alikuwa mtu nadhifu sana
akipendelea kuvaa English suit. Ama kwa hakika Mzee Philipo Sawani ana mambo
mengi sana aliyochangia kwa Kihesa na maisha ya wengi tukisema tuyaandike yote hapatoshi.
No comments:
Post a Comment