Pages

Sunday, October 7, 2012

WAZEE WA KIHESA -2-MZEE ISAYA KIGAHE

MFARANYAKI CLUB
Mzee huyu wa kabila la Kibena ambaye mpaka leo yupo pale Kihesa, ni mmoja ya wazee waliofika eneo la Kihesa miaka ya 1940. Ukiachaa mwanae wa kwanza Gerald Isaya Kigahe ambaye amefariki miezi michache iliyopita, Mzee huyu alikuwa na mwanae  aliyeitwa Naftari Isaya Kigahe aliyefariki takribani miongo miwili iliyopita. Naftari  alikuwa JEMBE kwa wana kihesa, huyu bwana ndio mmoja wa wawaanzilishi wa lile eneo la Mkimbizi ki ujenzi na likaitwa kwa Kigahe. Moja ya vitu ambavyo vilimgalimu Naftari kuanza kukaa eneo hili ni kuvamiwa na majambazi na kupigwa risasi, aliuguwa na kupona majeraha na kuendelea na shughuli zake kama kawaida. 
Naftari Kigahe ndiye mwenye watoto akiwemo Rogers, Christina, Ganma na mkewe se Msamba maarufu Mama Kigahe bado yupo, Mkimbizi kwa Kigahe anaendesha biashara zake. Kwa waliosoma shule ya msingi ya Chemchem , miaka hiyo ikiitwa Consolata Primary school watamkumbuka Naftari kuwa alikuwa ndiye alikuwa mpiga ngoma kubwa katika bendi ya shule miaka hiyo. Bendi iliyokuwa chini ya Mwalimu Daudi Luhanga.

No comments:

Post a Comment

STAT COUNTER