Mzee huyu wa kabila la Kibena ambaye mpaka leo yupo pale Kihesa, ni
mmoja ya wazee waliofika eneo la Kihesa miaka ya 1940. Ukiachaa mwanae wa kwanza Gerald Isaya Kigahe ambaye amefariki miezi michache iliyopita, Mzee huyu alikuwa na
mwanae aliyeitwa Naftari Isaya Kigahe aliyefariki takribani miongo miwili
iliyopita. Naftari alikuwa JEMBE kwa wana kihesa, huyu bwana ndio
mmoja wa wawaanzilishi wa lile eneo la Mkimbizi ki ujenzi na likaitwa kwa Kigahe. Moja ya
vitu ambavyo vilimgalimu Naftari kuanza kukaa eneo hili ni kuvamiwa na
majambazi na kupigwa risasi, aliuguwa na kupona majeraha na kuendelea na
shughuli zake kama kawaida. Naftari Kigahe
ndiye mwenye watoto akiwemo Rogers, Christina, Ganma na mkewe se Msamba maarufu Mama Kigahe bado yupo, Mkimbizi kwa Kigahe anaendesha biashara zake. Kwa waliosoma shule ya msingi ya Chemchem , miaka hiyo ikiitwa Consolata Primary school watamkumbuka Naftari kuwa alikuwa ndiye alikuwa mpiga ngoma kubwa katika bendi ya shule miaka hiyo. Bendi iliyokuwa chini ya Mwalimu Daudi Luhanga.
No comments:
Post a Comment