Jana tarehe 4 Novemba 2012, kulifanyika kikao kingine cha WanaKihesa, Katika hali ambayo inaonekana jambo la kukusanyika kwa Wana Kihesa ni jambo zuri mkutano wa jana ulikuwa na washiriki wengi kuliko mikutano ya awali, jambo ambalo ni jambo zuri sana kwani uzoefu unaonyesha kuwa mikutano ya aina hii huanza na watu wengi kisha wakapungua kila kikao na hatimae kufa kabisa kwa ushirikiano huo. Kamati mbalimbali zilizochaguliwa nazo zinaendelea vizuri kwani maandalizi ya Tamasha kubwa la WanaKihesa yamekwisha kamilika kwa asilimia 80. Kikao kijacho kimepangwa kuwa tarehe 18/11/2012.
Moja ya mambo yaliyofurahisha katika kikao ni kuwepo kwa wajukuu wa Mzee Mfaranyaki Cilla na Kidunu, kweli mkusanyiko huu umekuwa wa furaha kubwa kwani kuna wengi wanaokutana kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi , wengine kukutana kwa mara ya kwanza toka walipokuwa watoto, ni furaha tu. Wadau mnakaribishwa katika kikao kijacho katika tarehe iliyotajwa, katika ukumbi wa hoteli ya KGB pale Riverside Ubungo.
Sunday, November 4, 2012
Thursday, November 1, 2012
MZEE MBIGILI AFARIKI DUNIA LEO 1/11/2012 JIJINI DAR ES SALAAM
WAZEE WETU WOTE HAWA WAWILI SASA NI MAREHEMU. MZEE MBIGILI AKIWA KWENYE KOTI JEUSI NA PADRI MWOGOFI. MZEE MBIGILI AMEFARIKI LEO 1/11/2012 SAA NNE ASUBUHI JIJINI DAR ES SALAAM. TARATIBU ZINAFANYIKA ILI KUWEZA KUSAFIRISHA MWILI WA MAREHEMU KWENDA IRINGA KESHO.
MUNGU AWALAZE PEMA PEPONI AMEN
Tuesday, October 23, 2012
PROFESOR JAIROS MATOVELO MWAMPOGOLE na MWAMBA KASONGO MUNYAMWANI
MWAMBA KASONGO MUNYAMWANI
Mwana Kihesa huyu, alikuwa pilot wa ndege wa kwanza kutoka Kihesa, hii ilikuwa mwanzoni mwa 1970. Mwamba alikuwa ni mtoto pekee wa mmoja wa waanzilishi wa Kihesa Mzee Mnyamwani Kasongo. Mzee huyu mwenye asili ya ya mji wa Kisangani katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo alitinga Kihesa mwishon wa miaka ya 50. Ukoo huu ilizimika duniani baada ya Mwamba, Mama Mwamba, Mzee Mnyamwani, na mkee wake wa pili Binti Mussa wote kutangulia mbele ya haki.
Mwana Kihesa huyu, alikuwa pilot wa ndege wa kwanza kutoka Kihesa, hii ilikuwa mwanzoni mwa 1970. Mwamba alikuwa ni mtoto pekee wa mmoja wa waanzilishi wa Kihesa Mzee Mnyamwani Kasongo. Mzee huyu mwenye asili ya ya mji wa Kisangani katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo alitinga Kihesa mwishon wa miaka ya 50. Ukoo huu ilizimika duniani baada ya Mwamba, Mama Mwamba, Mzee Mnyamwani, na mkee wake wa pili Binti Mussa wote kutangulia mbele ya haki.
++++++++++++++++++++++++++++++++++
PROFESOR JAIROS MATOVELO MWAMPOGOLE
Mwana Kihesa huyu mtoto wa mama Se Uhagile ni msomi aliyebobea na ni muhadhiri pale chuo cha SAU ama kwa hakika kama si Profesor pekee toka Kihesa basi ni mmoja wa maprofesor wachache toka Kihesa. Alikuwa mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Lugalo katika miaka ya 70, alikuwa na tabia ya kusoma sana na pale alipotaka kupumzika basi rafiki zake wakubwa walikuwa Edson Mwamwani, Anderson Mwanyato na Ahmed Wanguvu wakitumia muda wao kucheza Bumping kwa wimbo wa Kung Fu Fighting, hapo ni mpaka jasho liwatoke.
MATAYARISHO YA SIKU YA WANAKIHESA YAPAMBA MOTO
Katika kikao cha wanaKihesa cha kutayarisha siku ya wanakihesa tarehe 2/12/2012, wanaKihesa waliokusanyika siku hiyo waliweza kukusanya shilingi laki
saba cash. Wajumbe wa kikao wamekubaliana kuwa kikao kijacho cha tarehe 4/11/2012 kuwa ni
muhimu sana watu wengi kufika kwani ndicho kitatoa picha kamili ya maandalizi
ya ya tamasha.
Pia tarehe 22/10/2012 matangazo ya tamasha yata anza kurushwa hewani rasmi na vituo vya Country Fm Iringa, na siku chache baadae vituo vya Clouds na Radio Free Africa vitaanza kutangaza taarifa za tamasha hilo.
Pia tarehe 22/10/2012 matangazo ya tamasha yata anza kurushwa hewani rasmi na vituo vya Country Fm Iringa, na siku chache baadae vituo vya Clouds na Radio Free Africa vitaanza kutangaza taarifa za tamasha hilo.
SETTI METUSALA SINZIALA MWAMOTTO na ANDERSON ZABRON MWANYATO
SETTI METUSALA SINZIALA MWAMOTTO ni mwana Kihesa ambaye pia ni mkurugenzi wa MAJEMBE AUCTION MART ni
mtoto wa kwanza wa mmoja wa wazee waanzilishi wa kihesa Methusela
Mwamotto .
Setti ameajiri vijana, wazee na wakina mama wengi kutoka Kihesa kwenye kampuni yake ya Majembe. Setti amekuwa akijitolea kujenga na kukarabati makanisa, misikiti na kuwasaidia kwa matibabu, misiba , na kadhalika ya watu wengi wa Iringa.
Setti ameajiri vijana, wazee na wakina mama wengi kutoka Kihesa kwenye kampuni yake ya Majembe. Setti amekuwa akijitolea kujenga na kukarabati makanisa, misikiti na kuwasaidia kwa matibabu, misiba , na kadhalika ya watu wengi wa Iringa.
ANDERSON ZABRON MWANYATO, mwanafunzi wa Katibu Mkuu wa zamani wa CCM ndugu Philip Mangula ni msomi wa darasa la 7 tu. lakini mambo aliyoyafanya enzi za uhahi wake ni kama mtu mwenye PHD. Anderson Mwanyato ni mtoto wa 4 wa mama Sekinyunyu na Mzee Z.K Mwanyato.
Ndiye alikuwa mkurugenzi wa Comfort
Enterprises
ambayo inamiliki hotel ya Comfort Kitonga, akishirikiana na ndugu zake wawili hayati Joshua na Alex. Alitoa mchango mkubwa wa kijamii mkoani Iringa
Mdogo wake Robert anasema anamkumbuka kwa kuwa mtu wa kuweza kushaurika, kwani yeye ndiye aliyemshauri ujenzi ule wa hotel porini Wanamuziki Hayati Ndala Kasheba na King kiki ndio waliosindikizana na Robert ili kupiga katika uzinduzi wa hoteli ile 1993. Comfort hotel ipo chini ya mkurugenzi pekee aliyebaki hai, Alex Zabron Mwanyato.
ambayo inamiliki hotel ya Comfort Kitonga, akishirikiana na ndugu zake wawili hayati Joshua na Alex. Alitoa mchango mkubwa wa kijamii mkoani Iringa
Mdogo wake Robert anasema anamkumbuka kwa kuwa mtu wa kuweza kushaurika, kwani yeye ndiye aliyemshauri ujenzi ule wa hotel porini Wanamuziki Hayati Ndala Kasheba na King kiki ndio waliosindikizana na Robert ili kupiga katika uzinduzi wa hoteli ile 1993. Comfort hotel ipo chini ya mkurugenzi pekee aliyebaki hai, Alex Zabron Mwanyato.
Tuesday, October 16, 2012
WAJUE WAZEE WA KIHESA 6
MZEE ERNEST MWANDANZI
Mzee huyu Mhehe wa Mufindi aliyestaafu uaskari akiwa na cheo cha Inspekta, ni mmoja wa wanzilishi wa Kihesa, alifanikiwa kuwa moja ya madiwani wa eneo hili. Mzee Ndanzi ndiye baba mzazi wa Gerald Ndanzi wa Majembe Auction Mart.
Mzee huyu Mhehe wa Mufindi aliyestaafu uaskari akiwa na cheo cha Inspekta, ni mmoja wa wanzilishi wa Kihesa, alifanikiwa kuwa moja ya madiwani wa eneo hili. Mzee Ndanzi ndiye baba mzazi wa Gerald Ndanzi wa Majembe Auction Mart.
MZEE MARTIN MLOWE
Mzee huyu Mbena wa Kifanya - Njombe ni
mmoja wa waanzilishi wa Kihesa. Pamoja na kujishughulisha na kilimo eneo la
Mangao Ismani, aliku.wa na bucha
pale Kihesa alibarikiwa kupata watoto wengi kama Gaspar, Oscar, Gerard,
mtoto wa mwisho wa kiume Afred Mlowe alikuwa mchezaji kiungo wa Kihesa Stars,
mchezaji mwenzie Robert Nyato hudai kuwa anamfananisha na Steven Gerald Alfred
ndiye mtunza hazina wa Umoja wa wana Kihesa. Kwa sasa ni mfanyakazi wa Manispaa
ya kinondoni
Leo
tutazungumzia wasifu wa wazee wa kihesa ambao ni wazazi wa ndugu Faustini Mdesa
cosmas na tutamzungumzia Mzee wa kijana mhamasishaji wa siku ya wana
kihesa Ali mduba.
MZEE COSMAS MDESA
Mzee huyu Mhehe wa Ifunda ni mwana Kihesa ambaye alijishughulisha na kilimo huko Kihologota Ismani akiwa na mjomba wake mzee Mwang’ingo. Mzee huyu ndiye baba mzazi wa mwenyekiti wa maandalizi ya siku ya wana kihesa Ndugu Faustine Cosmas Mdesa
MZEE JIMMY MWAMBAGO
Mzee huyu Mbena wa Njombe ambaye alitinga Kihesa 1962, akitokea Tanga ambako alikuwa akifanya kazi upimaji na ramani. Mzee Jimmy alijiunga na kufanya kazi TANCUT na kusaafu mwishoni mwaka 1979. Bingwa huyu ambaye ni mzazi wa mwenyekiti wa Mkusanyiko wa wana Kihesa wa dar es Salaam Ndugu Nordrick Mwambago. Kwa sasa mzee Mwambago bado yupo anaishi Kihesa nyumbani kwake. Mwanae Nodrick Jimmy Mwambago ndie mwenyekiti wa wana KIHESA na mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya siku ya wana Kihesa 2/12/2012
MZEE COSMAS MDESA
Mzee huyu Mhehe wa Ifunda ni mwana Kihesa ambaye alijishughulisha na kilimo huko Kihologota Ismani akiwa na mjomba wake mzee Mwang’ingo. Mzee huyu ndiye baba mzazi wa mwenyekiti wa maandalizi ya siku ya wana kihesa Ndugu Faustine Cosmas Mdesa
MZEE JIMMY MWAMBAGO
Mzee huyu Mbena wa Njombe ambaye alitinga Kihesa 1962, akitokea Tanga ambako alikuwa akifanya kazi upimaji na ramani. Mzee Jimmy alijiunga na kufanya kazi TANCUT na kusaafu mwishoni mwaka 1979. Bingwa huyu ambaye ni mzazi wa mwenyekiti wa Mkusanyiko wa wana Kihesa wa dar es Salaam Ndugu Nordrick Mwambago. Kwa sasa mzee Mwambago bado yupo anaishi Kihesa nyumbani kwake. Mwanae Nodrick Jimmy Mwambago ndie mwenyekiti wa wana KIHESA na mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya siku ya wana Kihesa 2/12/2012
Subscribe to:
Posts (Atom)