Pages

Sunday, November 4, 2012

KIKAO CHA WANAKIHESA CHAFANA

Jana tarehe 4 Novemba 2012, kulifanyika  kikao kingine cha WanaKihesa, Katika hali ambayo inaonekana jambo la kukusanyika kwa Wana Kihesa ni jambo zuri mkutano wa jana ulikuwa na washiriki wengi kuliko mikutano ya awali, jambo ambalo ni jambo zuri sana kwani uzoefu unaonyesha kuwa mikutano ya aina hii huanza na watu wengi kisha wakapungua kila kikao na hatimae kufa kabisa kwa ushirikiano huo. Kamati mbalimbali zilizochaguliwa nazo zinaendelea vizuri kwani maandalizi ya Tamasha kubwa la WanaKihesa yamekwisha kamilika kwa asilimia 80. Kikao kijacho kimepangwa kuwa tarehe 18/11/2012.
 Moja ya mambo yaliyofurahisha katika kikao ni kuwepo kwa wajukuu wa Mzee Mfaranyaki Cilla na Kidunu, kweli mkusanyiko huu umekuwa wa furaha kubwa kwani kuna wengi wanaokutana kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi , wengine kukutana kwa mara ya kwanza toka walipokuwa watoto, ni furaha tu. Wadau mnakaribishwa katika kikao kijacho katika tarehe iliyotajwa, katika ukumbi wa hoteli ya KGB pale Riverside Ubungo.

No comments:

Post a Comment

STAT COUNTER