Pages

Thursday, October 11, 2012

KABATI KATIBA STAR SEARCH- KUZINDULIWA JUMAMOSI


 Katika kuhamasiisha vijana wa Iringa kushiriki katika kutoa mchango wa mawazo kuhusu katiba mpya na pia katika kutafuta vipaji vya vijana wa Iringa, Mbunge wa Viti Maalumu kupitia CCM Mheshimiwa Ritha Kabati, Jumamosi hii tarehe 13 Oktoba, atazindua  KABATI KATIBA STAR SEARCH.  Shughuli hiyo itaanza kwa elimu ya Katiba itakayotolewa kwa washiriki ambao mpaka sasa 400 wamekwisha jiandikisha, na hawa watapewa elimu kuhusu katiba iliyoko na mategemeo ya katiba ijayo ili kuhamasisha mchango wa mawazo toka vijana wa Iringa. Washindi wa KABATI KATIBA STAR SEARCH watapatiwa zawadi mbalimbali ikiwemo nafasi ya kurekodi nyimbo mbili na video zake, kwa mshindi wa kwanza, mshindi wa pili atapata nafasi ya kurekodi nyimbo mbili, mshindi wa tatu atarekodi wimbo mmoja na washindi wa nne na wa tano watafanya wimbo mmoja kwa kushirikiana. Mheshimiwa Kabati aliomba vijana wajitokeze kwa wingi kwani watapata mengi katika shughuli hii inayotegemea kuchukua mwezi mmoja. Wasanii kadhaa ambao ni wenyeji wa Iringa wamekwisha onyesha nia ya kutoa ushirikiano katika shughuli hii yote.

Tuesday, October 9, 2012

MSIBA KIHESA CHRISTOPHER MMASI HATUNAE TENA

CHRISTOPHER MMASI KAKA WA PATRICIA MMASI AMEFARIKI USIKU HUU HUKO IRINGA. MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI AMINA
KWA MICHANGO MBALIMBALI YA RAMBIRAMBI UNAWEZA KUTUMA KUPITIA SIMU NAMBA 0754591929-DEVOTA MSILU
TAARIFA ZIMELETWA NA ROBERT MWANYATO

INDONYA NGOMI KUMWANI TWIYANGALILE

Kwa kuwa wameweka kidhungu ngoja tuweke Kiswahili kwa kifupi, TAHADHARI YA MVUA KUBWA NA UPEPO MKALI, KATI YA 8TH OKTOBA NA 11 OKTOBA 2012. MAENEO HUSIKA NI MIKOA YA DAR ES SALAAM, MOROGORO, PWANI, NA VISIWA VYA UNGUJA NA PEMBA. KUNAWEZEKANA KUWEKO NA MVUA KUBWA YA KATI YA 50mm na 100mm KATIKA KIPINDI CHA MASAA 24,

Monday, October 8, 2012

WAZEE WA KIHESA 3- MZEE LOTTI LUPEMBE

-->   Mzee huyu wa kabila la Kibena alikuwa mkulima wa kawaida sehemu za Isimani kama ilivyokuwa kawaida  ya wazee wengi waanzilishi wa Kihesa. Baada ya mavuno mazuri walijenga nyumba zao  Kihesa. Mzee lotti alijizolea umaarufu  Kihesa kwa tabia yake ya kujitolea kupita asubuhi na mapema karibu kila mtaa na kutoa matangazo kwa wananchi , kwa mfano mtoto kapotea, ama kuna msiba umetokea n.k, kutokana na umaarufu huo wa Mzee Lotti, pale kihesa kuna mtaa unaitwa kwa LOTTI LUPEMBE .

Sunday, October 7, 2012

WAZEE WA KIHESA -2-MZEE ISAYA KIGAHE

MFARANYAKI CLUB
Mzee huyu wa kabila la Kibena ambaye mpaka leo yupo pale Kihesa, ni mmoja ya wazee waliofika eneo la Kihesa miaka ya 1940. Ukiachaa mwanae wa kwanza Gerald Isaya Kigahe ambaye amefariki miezi michache iliyopita, Mzee huyu alikuwa na mwanae  aliyeitwa Naftari Isaya Kigahe aliyefariki takribani miongo miwili iliyopita. Naftari  alikuwa JEMBE kwa wana kihesa, huyu bwana ndio mmoja wa wawaanzilishi wa lile eneo la Mkimbizi ki ujenzi na likaitwa kwa Kigahe. Moja ya vitu ambavyo vilimgalimu Naftari kuanza kukaa eneo hili ni kuvamiwa na majambazi na kupigwa risasi, aliuguwa na kupona majeraha na kuendelea na shughuli zake kama kawaida. 
Naftari Kigahe ndiye mwenye watoto akiwemo Rogers, Christina, Ganma na mkewe se Msamba maarufu Mama Kigahe bado yupo, Mkimbizi kwa Kigahe anaendesha biashara zake. Kwa waliosoma shule ya msingi ya Chemchem , miaka hiyo ikiitwa Consolata Primary school watamkumbuka Naftari kuwa alikuwa ndiye alikuwa mpiga ngoma kubwa katika bendi ya shule miaka hiyo. Bendi iliyokuwa chini ya Mwalimu Daudi Luhanga.

MBUNGE WA ZAMANI WA MUFINDI AFARIKI DUNIA

Habari zilizotufikia muda si mrefu ni kuwa Mbunge wa zamani wa  Jimbo la Mufindi  kusini, Mhe.Benito Malangalila amefariki dunia  jana katika hospitali ya wilaya ya Mufindi mjini Mafinga mkoani  Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi Amina.

WAZEE WA KIHESA -1-MZEE PHILIPO SAWANI

Mzee huyu wa kabila la Kikinga ambaye ni mmoja wa waanzilishi wa Kihesa alikuwa mkulima eneo la Ngano Isimani. Huku akiendesha biashara ya duka na bar hapo KIHESA katika nyumba yake ya kisasa kabisa. Wazee matajiri wa mji wa Iringa mfano Mzee Mwaitebele, Mzee Idd Mwangubi, Mzee Zabron Mwanyato pamoja na wafanya kazi maofisa kama Mzee Asam Sajio Kaduma walipenda kunywa kwenye bar ya Mzee Sawani. Lakini pia alipokuwa Mwenyekiti wa Tanganyika African Parents Association (TAPA) wa wilaya na alinunua jengo kwa pesa zake na kulifanya shule ya TAPA ambayo kwa sasa inaitwa Shule ya Msingi Mtwivila. Na mwalimu wa shule hiyo wa kwanza alikuwa Mwalimu Edward Chaula ( Baba Kichupa ) na Joseph Msandi ambao mishahara yao ililipwa na mzee Philipo Sawani. Jully Sawani ni mtoto wa Mzee Sawani ambaye alikuwa diwani wa kwanza Kihesa. Mzee Sawani alikuwa  mtu nadhifu sana akipendelea kuvaa English suit. Ama kwa hakika Mzee Philipo Sawani ana mambo mengi sana aliyochangia kwa Kihesa na maisha ya wengi tukisema tuyaandike yote hapatoshi.

STAT COUNTER