Pages

Tuesday, October 16, 2012

WAJUE WAZEE WA KIHESA 6


MZEE ERNEST MWANDANZI 
 Mzee huyu Mhehe wa Mufindi aliyestaafu uaskari akiwa na cheo cha Inspekta, ni mmoja wa wanzilishi wa Kihesa, alifanikiwa kuwa moja ya madiwani wa eneo hili.  Mzee Ndanzi ndiye baba mzazi wa Gerald Ndanzi wa Majembe Auction Mart.

MZEE MARTIN MLOWE 
 Mzee huyu Mbena  wa Kifanya - Njombe  ni mmoja wa waanzilishi wa Kihesa. Pamoja na kujishughulisha na kilimo eneo la Mangao Ismani, aliku.wa na bucha  pale Kihesa alibarikiwa kupata watoto wengi kama Gaspar, Oscar, Gerard, mtoto wa mwisho wa kiume Afred Mlowe alikuwa mchezaji kiungo wa Kihesa Stars, mchezaji mwenzie Robert Nyato hudai kuwa anamfananisha na Steven Gerald Alfred ndiye mtunza hazina wa Umoja wa wana Kihesa. Kwa sasa ni mfanyakazi wa Manispaa ya kinondoni 

Leo tutazungumzia wasifu wa wazee wa kihesa ambao ni wazazi wa ndugu Faustini Mdesa cosmas na tutamzungumzia Mzee wa kijana mhamasishaji wa siku ya wana kihesa  Ali mduba.

MZEE COSMAS MDESA
 Mzee huyu Mhehe wa Ifunda ni mwana Kihesa ambaye alijishughulisha na kilimo huko Kihologota Ismani akiwa na mjomba wake mzee Mwang’ingo. Mzee huyu ndiye baba mzazi wa mwenyekiti wa maandalizi ya siku ya wana kihesa Ndugu Faustine Cosmas Mdesa

MZEE JIMMY MWAMBAGO
 Mzee huyu Mbena wa Njombe ambaye alitinga Kihesa 1962, akitokea Tanga ambako alikuwa akifanya kazi upimaji na ramani. Mzee Jimmy alijiunga na kufanya kazi TANCUT na kusaafu mwishoni mwaka 1979. Bingwa huyu ambaye ni mzazi wa mwenyekiti wa Mkusanyiko wa wana Kihesa wa dar es Salaam Ndugu Nordrick Mwambago. Kwa sasa mzee Mwambago bado yupo anaishi Kihesa nyumbani kwake. Mwanae  Nodrick Jimmy Mwambago ndie  mwenyekiti wa wana KIHESA na mwenyekiti wa  kamati ya maandalizi ya siku ya wana Kihesa 2/12/2012

KABATI KATIBA STAR SEARCH YAPATA 20 BORA

Jumamosi tarehe 13 Oktoba katika ukumbi wa Welfare Center, mambo makubwa mawili yalifanyika, kwanza vijana wengi walioshiriki na wale waliokuja kufuatia Kabati Katiba Star Search walipata elimu nzuri ya Katiba ya Tanzania. Na pili ilikuwa burudani kwa kwenda mbele kutoka kwa vijana walioshiriki Star Search kuonyesha vipaji vyao. Vijana 150 waliweza kujitokeza kuonekana mbele ya jopo la majaji
majaji  Eddo Bashir (Ebony Fm), Temmy Mahondo (Country Fm), Dj Ammy Yeyo (Country Fm ), Agnes Anderson (Ebony Fm) na Dj Muba wa (Ebony Fm) . Mchujo uiofanyika baada ya hapo uliwezesha vijana 20 kuingia katika Top Twenty ya mpambano huo. Tarehe 27 Oktoba ndipo itakapoingia awamu ya pili ya shindano hili na Top Ten kupatikana.

Friday, October 12, 2012

TEMBELEA KIHESA KWA PICHA 2







JOHN BAKERY(RIP), MWAMBA, KITIME


WAZEE WA KIHESA-5-MZEE RUBENI NYALUSI

Klerruu
Mzee huyu Mbena wa Lupembe alikuwa fundi stadi wa ujenzi na kuongoza umoja wa wajenzi Kihesa yeye akiwa mwenyekiti. Mzee huyu pia alijishughulisha na kilimo sehemu za Ngano Ismani, sambamba na Mzee Philipo Sawani. Hayati Mzee Nyalusi ndiye baba mzazi wa mchezaji mahiri wa ile timu maarufu Kihesa Stars Simoni Nyalusi.
Mchezaji huyu aliyekuwa na vituko vingi uwanjani, mpaka hivi leo bado yupo Kihesa akijishughulisha na ufundi ujenzi. Miongoni mwa vituko ambavyo mtoa habari hii Bwana Robert Nyato anasema hatasahau ni kitendo cha kupewa kadi nyekundu na refarii baada ya kumvuta pua mshika kibendera marehemu Bruda Modestus katika mechi kati ya Kihesa Stars na Lipuli zote za Iringa, refa  Mzee Maselenge alimtoa nje. Kituko kingine ni akiwa kama mtazamaji kwenye mashindano ya vyuo pale Kleruu aliingia uwanjani na kuifungia bao timu ya Kleruu na kusababisha mchezo kusimama takribani dakika 20 na wachezaji wa  timu ile ya Chuo cha Mbeya kuanza kumfukuza Simoni bila mafanikio yoyote.

TEMBELEA KIHESA KWA PICHA 1

Kama uliwahi kuwa mkazi wa Kihesa picha hizi zitakukumbusha mengi








WAZEE WA KIHESA-4-MZEE ZABRON KIPANDULE MWANYATO

--> Mzee huyu Mbena wa Kidegembye alitinga kihesa 1935. kwa miaka kadhaa aliishi nyuma ya mlima Mafifi kabla ya kuja kuwa mmoja wa waanzilishi wa Kihesa.  Kabla hajajulikana kama mkulima stadi alikuwa fundi washi, ndipo baadae akajishughulisha na kilimo kupitia mashamba makubwa aliokuwa nayo maeneo ya Chamdindi na Kifuluto kule Isimani. 
Mzee huyu akiwa na mkewe  mama Sekinyunyu alifikia uwezo wa  kumiliki  magari na matrekta. Mtoto wake wa kwanza  alikuwa Waston maarufu kwa jina la Fwasi Kilega ambaye kwa sasa ni marehemu na wengine kama Matata(Mbinu), Geofrey, Manase, Yotema wapo bado Kihesa mpaka leo.

STAT COUNTER