-->
Mzee huyu Mbena wa Kidegembye alitinga kihesa 1935. kwa miaka kadhaa aliishi
nyuma ya mlima Mafifi kabla ya kuja kuwa mmoja wa waanzilishi wa Kihesa. Kabla hajajulikana kama
mkulima stadi alikuwa fundi washi, ndipo baadae akajishughulisha na kilimo kupitia mashamba makubwa aliokuwa nayo maeneo ya Chamdindi na Kifuluto kule Isimani.
Mzee
huyu akiwa na mkewe mama Sekinyunyu alifikia uwezo wa kumiliki magari na
matrekta. Mtoto wake wa kwanza alikuwa Waston maarufu kwa jina la Fwasi Kilega
ambaye kwa sasa ni marehemu na wengine kama Matata(Mbinu), Geofrey, Manase, Yotema wapo
bado Kihesa mpaka leo.
No comments:
Post a Comment