Kama
nilivyoeleza katika makala zilizopita, wale
watu weupe waliowatimua Wategeta walikuwa pia wakifanya biashara ya
kuuza watumwa. Koo nyingi
za Kihehe hazikukubali kuuuzwa hivyo wengine waliona heri wauwawe, wengine
waligoma kula hivyo kufa wakiwa katika masafara wa kuelekea pwani, na wengine
walikimbia mbali kutoka maeneo yao ya asili.
Tuliona jinsi kabila la Wanyakyusa lilivyopatikana kutokana na
kusambaratika huko. Wagogo pia ni kabila lilitokana na fujo hizo. Koo
mbalimbali za Wahehe walikimbilia kaskazini na kufika mpaka sehemu inaitwa
Mkofa kando ya mto Lyambangali, wakawa
wanatafuta namna ya kuvuka kwenda upande wa pili, sehemu moja
wakakuta gogo kubwa limeanguka na kulala juu ya mto na kutengeneza aina ya
daraja, hivyo wakaweza kuvuka kumkimbia adui, kwa kukumbuka kuvuka huko, wahehe
wale walijiita Vanyagogo, jina ambalo baadae likafupishwa kuwa Wagogo.
Wagogo wengi
kwa kukumbuka walikotoka huwaita Wahehe wajomba zao.
Kuna
simulizi za kale kuwa Warangi walitokana na watu watu weupe waliohamia
Uheheni kutoka Usambara.
Wakati ule
koo kadhaa zilizokuwa zikiishi karibu na bahari ya Hindi zilijikuta zikiwa na
machotara wengi wa Kiarabu na baadae waKireno. Watu hawa weupe toka Usambara
walikuja kuishi sehemu ya Ugunda iliyokuwa ikiitwa Ilamba na wengine kuhamia
Usagala.
Kuna Wasagala wa zamani walikuwa weupe na
wanaume wakawa na nywele nyingi mikononi na kifuani na walikuja kuwa na muitiko
au mwidikiso wa Mnyakami, inawezekana walikuwa na uhusiano na Wakami wa Ulugulu. Hawa watu
weupe walienea sehemu nyingi za Uhehe, Ubena
na Ukimbu. Wale waliobaki Ugunda, Wahehe
walianza kuwaita Valangi. Valangi hawa
na ndugu zao Wanyiramba walikuja kuhamia maeneo ilipo Singida sasa. Kuna wakati
wajukuu wa Valangi hawa waliamua kurudi kwao Uheheni, lakini karibu na Dodoma wakakutana
na ukoo wa Wadongwe waliokuwa chini ya Kiongozi wao Muyovela, vita kali
ikaanza wakashindwa na wakalazimika
kukimbilia ilipo Kondoa sasa na huko wakaishi na kuongezeka na kuwa kabila
kubwa.
Makundi
mengine ya watu weupe yalisonga mbele
mpaka Ukimbu, kundi jingine likahamia
sehemu za Ilembula, kundi jingine likahamia kwa muda sehemu za Wasa, kisha
kuelekea Malangali.
Kundi hili
ndilo linalosemekana liliingiza kilimo cha kulima mahala kwenye majani kwa
kugeuza udongo na kutengeneza matuta kwa kufukia majani. Majani yale yaliachwa
kwa muda ili yaoze na kisha ndipo mbegu hupandwa.
Kilimo hiki
kilileta mazao mengi, killimo hiki kiliitwa Malongo, na sehemu ile ya malangali
ikaitwa Ilongo.
Wahehe huita mavuno
mengi kuwa ni Sanga. Katika
sehemu hiyo ya Ilongo kukaweko na kundi fulani la wakulima waliokuwa hodari wa
kulima malongo na hivyo kuwa wanapata mavuno mengi wakaanza kuitwa Vanyasanga, mafanikio ya Vanyasanga yakwaletea maadui na wakaamua
kuhamia sehemu za Ukinga na Uwanji, na ndio chanzo cha koo za Sanga huko Ukinga
na Uwanji.
Ukoo wa Kihaule pia husema walitokea Ilongo,
na hata mwitiko wa binti wa kina Kihaule ni Nyamalongo. Wazee wa Upangwa husema
kina Kihaule wa kwanza kuingia huko walikuwa weupe na walileta kilimo cha
malongo, pia ndio waliokuja kusitisha mila ya kumzika mke akiwa mzima mzima
kama mumewe amefariki, mila hii hata Wahehe awali walikuwa nayo.
Sunday, July 31, 2022
UNAJUA KUWA ZAMANI MHEHE MWANAUME AKIFA ANAZIKWA NA MKEWE ALIYE HAI?
Saturday, July 30, 2022
WANYAKYUSA WALITOKA UHEHENI
Vanu velu au watu weupe waliotoka Kilwa waliingia nchi ya Uheheni kwa amani na wakaendelea kuishi kwa amani na hatimae kuwa sehemu ya wenyeji, mfano nilioutoa ni wakina Kiwhele.
Lakini kuna kundi jingine la
watu weupe hawa waliingia kutoka kaskazini na kuingia katika eneo lililoitwa
Ugunda, wenyeji wa Ugunda walikuwa ni Wategeta, habari zao nilikwisha
zizungumzia awali. Jina la Ugunda lilitokana na babu yao mmoja aliyeitwa
Mugunda. Eneno la Ugunda kwa sasa
linaitwa Image na tutaelezana chanzo cha jina hilo baadae. Kama mnakumbuka, niliwaeleza
kuwa Wategeta walikuwa wafua chuma wazuri sana na walikuwa watu walioishi kwa
mpangilio mzuri katika kazi yao hiyo, pia niliwaambia kuwa walikuwa ni watu
wenye maungo makubwa yenye afya hawakuwa watu wa mchezo. Kuna kundi moja la
Wahumma kutokea aidha Pawaga au Izazi, liliwashambulia Wategeta hawa ili
kuwanyang’anya ng’ombe. Pamoja na Wahuma kuwa na silaha za kutisha ,Wategeta
waliwakamata adui zao hao kwa mikono na kuanza kuwachanachana vipande.
Walimbakiza Muhumba mmoja tu nae walikata masikio wakamwachia aende kwao
akahadithie. Baada ya hapo Wategeta wakawa mara kwa mara wanawashambulia Wahuma
na kuwanyang’anya ng’ombe bila upinzani mkubwa.
Lakini hili kundi la watu weupe kutoka kaskazini liliwazidi sana nguvu
Wategeta. Wenyeji wengi wakalazimika kukimbia nchi yao na kukimbilia upande wa
iliko Pawaga sasa, wale maadui waliwafwata mpaka huko na kuwamaliza na
waliobaki kuwachukua watumwa na kwenda kuwauza Pwani. Mahala palipokamilisha
vita hiyo palikuja kuitwa Malikilo maana yake pa kumalizia. Siku hizi panaitwa
Kidali.
Wategeta
wengine walikimbia kaskazini na kufika mpaka ulipo sasa mpaka wa Kenya na
Uganda. Huko wakalikuta kabila la Wasamia na kuwashinda na kuwa watawala wao.
Hata siku hizi wajukuu zao hujiita Bahehe na kusema kuwa babu zao walitokea
Uheheni. Kundi jingine la Wategeta lilikimbilia Mahenge na baadae kuanza
kufuata bonde la Kilombelo kisha kuingia
Ubena na kuendelea na safari hadi Kaskazini mwa Ziwa Nyasa, wakaanza kuishi
sehemu waliyoiita Kavala, maana yake
peupe penye kuwaka jua, wakaendelea na kazi yao ya asili ya uhunzi.
Wengi wao walikuwa wa ukoo wa kina Chusi na wakawa watawala, jina lao likageuka
kuwa Chusa, Wagonde wakaligeuza jina
hilo kuwa Wanyachusa, au Wanyakyusa. Kuna Wanyakyusa ambao hatimae walirudi
Uheheni kwa mfano ukoo wa akina Kalinga, hawa walitumia majina kama
Kwilengilyova, yaani maji yangurumayo, wakikumbuka maporomoko ya maji katika sehemu walizopita
wakati wakisafiri wakifuata bonde la Kilombelo. Wengine wakijiita Magalamatitu,
wakikumbuka sehemu ambapo kulikuwa tambarare
ya ndege wengi weusi ambayo ipo
mpaka leo. Hawa watu weupe waliowafukuza Wategeta waliacha uzao wao katika nchi
ya Usagala. Wajukuu hawa wa Wasagala wa zamani, ambao hujulikana kama
Vanyikami, huwa na madai tofauti, wengine wakidai kuwa asili yao ni waarabu,
wengine wakidai asili yao ni wazungu. Wanahistoria wengi huona hiyo si rahisi
kwani wangekuwa Waarabu, lazima wangeanzisha dini ya Kiislamu na hali kadhalika
wangekuwa wazungu kungeletwa pia ukristu. Kinachodhaniwa ni kuwa Vanu velu hawa
walikuwa ni machotara au watu tu wenye ngozi angavu.
UNAJUA WAHEHE WALITOKEA WAPI 2 ? marekebisho
Wabena ndio chanzo cha Wahehe. Inasemekana jina la kabila hili lilitokana na kutofautiana katika mshangao na kabila lao mama la Wabena. Wahehe walikuwa wakishangaa kwa kusema He he, Wabena walikuwa wakishangaa kwa kusema khe khe. Baadaye Wahehe walitumia sauti hiyo hata wakati wakiwa vitani. Kama nilivyosema katika sehemu ya kwanza ya simulizi hii, makundi mawili ya wabena yaliondoka Nyumbanitu na kuelekea Kaskazini mashariki na kuja kuishi kwa muda Magharibi mwa ilipo Malangali sasa. Lakini tena kukaweko na mgawanyiko, kundi moja lilielekea bonde la Lyambangali na kuanzisha kabila la Wasangu , wakati kundi jingine likielekea upande wa pili na hili likaja kuwa chanzo cha Wahehe. Katika kugawanyika huku, sehemu waliyoanzia kugawanyika ikaitwa Igawilo maana yake penye kugawa nchi.
Kama ilivyokuwa katika tabia za Kibantu watu
hawa waliokuja kuitwa Wahehe awali waligawanyika katika koo mbalimbali, japo
inasemekana walikwisha anza kujitambulisha kama Wahehe. Kati ya koo maarufu walikuweko akina;
Vigawilo –
Hawa ni wale waliobaki pale Igawilo, na baadae wengine wakaaza kusambaa katika bonde la
Lyandembela na kuanza kuitwa Vilongo. Mwiko wao hawa ulikuwa bandama, jamaa wa
ukoo huu ni akina Kibodya na Mugandu.
Vahafiwa –
hawa walienea katika sehemu zinazoitwa siku hizi Tanangozi, welu, kalenga
Ntsihi, na maeneo yanayozunguka mji wa Iringa.
Kuna wakati
maeneo haya yalipata uhaba mkubwa wa mvua hivyo kukawa na njaa na hata watu
wengi wakafa kwa njaa, waliosalimika
walikuja kupata mwidikiso wa Vahafiwa
maana yake waliofiwa na wengine walikuwa na mwidikiso wa Mponela yaani
aliyepona njaa.
Wengine
walikuja kuitwa Vanyalugome kwa sababu ya desturi yao ya kutengeneza mitego ya
wanyama kwa kuchimba mahandaki.
Mwiko wao
hawa ilikuwa ni nyopolwa, Yaani mimba ya mnyama yoyote.
Labda niseme
hapa hapa kuwa mwiko maana yake hawaruhusiwi kamwe hata kuonja nyama hiyo.
Kati ya koo
zinazojulikana kutoka kundi hili ni akina Mugovano, Mukemangwa na mutono,
Vanyandevelwa-
maana yake wepesi kuchokozwa, makazi ya kundi hili yalikuwa kati ya barabara
mbili zilizoanzia Iringa, yaani ile ya kwenda
Dar es Salaam na ile ya kwenda Dodoma
.Awali nao
mwiko wao ulikuwa nyopolwa lakini walikuja kunyangwa nchi na kundi lililoitwa
Vanyamahuvi na kuja kutawaliwa nao.
Hawa Wanyamahuvi wakaja kutwaa jina la
Vanyandevela lakini wakaendeleza mwiko wao ambao ni ndege kanga, Ni vigumu siku
hizi kupambanua nani ni Mnyandevela wa awali na nani Mnyamahuvi wa awali
Vategeta
hawa walikuwa na umuhimu sana katika kabila la wahehe kwani walikuwa mafundi wa
kufua chuma.
Wategeta
ndio waliounda mikuki, mundu shoka na kadhalika. Wategeta waliishi karibu na
kila ukoo wa Wahehe na hasa sehemu zenye mchanga uliweza kutoa chuma, wengi
walikuwa warefu wenye maungo yenye afya na hivyo basi waliweza kufikia kutawala
katika sehemu nyingi walizokuwa wakiishi.
Wategeta
waligawana kazi, walikuwa na sifa ya kuwa wana mipangilio katika maisha
yao. Wale waliokuwa mabingwa wakutafuta
kuni kwa ajili ya mkaa wa kuyeyushia chuma waliitwa Vanyantsagala …nzagala ni
kuni, baadae walikuja kufupishwa na kuitwa Wasagala.
Wategeta ambao walikuwa na utaalamu wa
kuchagua mchanga bora kwa chuma waliitwa Vayunga, ambao ndio chanzo cha
Watsungwa. Kutokana majina haya
walipoenea na kuwa wengi sehemu waliyoenea Vayunga ikaitwa Utsungwa na walikoenea
Wasagala ikaitwa Usagala.
Mwiko wa Wategeta ni mato kwa Kiswahili
mbawala na wengine mwiko wao ni dundulu yaani twiga. Inasemekana waliamini kuwa
kwa kula nyama ya wanyama hao wangepata
ukoma ,kwani ngozi ya binadamu huwa na mabaka meupe kama twiga, kama ameambukizwa
ukoma.
Kati ya koo
za Wategeta maarufu ni Chusi na kina Mveyange
Wakilwa,,,
hawa waliitwa hivi kwa kuwa walitokewa Kilwa na kuingia sehemu inayoitwa siku
hizi Mufindi kwenye robo ya kwanza ya
karne ya 16. Yaani mwaka 1500. Hawa hawakutokana na Wabena kama Wahehe wengine.
Hawa
walikuwa na ngozi ya maji ya kunde na walikuwa na nywele nyingi mikononi na
kifuani. Nywele ambazo Wahehe huziita
Lyagi,hivyo Wakilwa pia wakaaitwa Vanyalyagi. Dalili hizi ziliwatofautisha na
wabantu wengine. Inasemekana walipokuwa badi Kilwa, walichanganyika na Wareno na Washirazi waliokuwa
tayari wametua Kilwa wakati huo.
Kati ya Wakilwa wa Uheheni ni akina Kihwele ambao walipoenea Uheheni walionyesha
kutengeneza vifaa vya chuma bora kuliko Wategeta. Huko Katanga Kongo kuna ukoo unaitwa Kiwele,
na kuna uwezekano kuwa ni ndugu wa Kihwele wa Uheheni kwani wote walikuwa
wakizika wafu wao kichwa kikielekea mashariki, kwa kukumbuka kwao Kilwa, ambayo iko mashariki mwa
Katanga na Uhehe pia,
NDONGWA SA KIHEHE -unaejua maana weka jina lako na maana kwenye comments
1. Muhwehwe luheko
2. Imbwa ndavila pasi ye nyisi.
3. Kwe wisagalila, ndemuyago ndaiwopola.
4. Ukwegi hanzu na malagala. (Mkwega
mahanzu na malagala)
5. Umulomo si kitegulo
6. Umpafi si muwulasi
7. Chalonzile mkwamilingwada, alakiwene
8. Uwudodi waikala
9. Kinyawihanga, kinawigafi, ulihuvila nda
10. Ulanonela ing'wale, nonelage ulutego.
11. Yeyigwafile, yayilya na masoli
12. Inyengo ing'angafu (inzugi) yadenyekye
muluwono
13. Mfumbika moto muhenge chusi kilaling'a
14. Apanya makukilo peyitonyite indonya
15. Imbwa sakwinava se sesisele
Thursday, July 28, 2022
UMUYAGO YE MWIYENDA
Umuyago ye mwiyenda mamaa
Umyago ye mwiyenda
Umuyago ye mwiyenda mama ye muhavi mulala
Gendeluwema mama
Gendeleuwema
Gendeluwema mama munyi yavene
Wednesday, July 27, 2022
HIVI UNAJUA WAHEHE WALITOKEA WAPI? FUATILIA HAPA
![]() |
Isimila |
Tukirudi nyuma kama miaka 11,000 iliyopita tuna ushahidi kuwa walikuweko binadamu ambao walitumia silaha za kuchonga mawe, kihistoria zama hizo hujulikana kama zama za mawe au stone age era.
Kilomita chache
kutoka mji wa Iringa, ukiwa unaelekea na
barabara kuu iendayo Mbeya, kuna sehemu inaitwa Isimila,
hapa katika bonde moja kubwa kunapatikana ushahidi wa
vipande vya mawe vilivyochongwa kwa ajili ya kazi mbalimbali hasa za uwindaji
katika zama hizo.
Wahehe walipopafahamu hapa ndipo wakapaita Isimila, jina
linalotokana na neno la Kihehe ‘simo’, maana yake fumbo. Kwani kuweko kwa
silaha zile za mawe kwa wahehe lilikuwa fumbo.
Ukiingia sehemu za Usagala kuna mlima uitwao Ikombagulu,
huku kuna pango ambako iko michoro ya zamani sana, kuonyesha kuwa pia kulikuwa
na watu waliokuwa na utamaduni wa michoro ya mapangoni.
Katika bhonde la mto Lya Ndembela kuna ushahidi wa kuishi
watu ambao Wahehe katika simulizi zao waliwaitwa Vanyidaha,
watu hawa waliacha
ushahidi wa utamaduni uliofanana sana na utamaduni wa Wairaki wa huko Mbulu,
kuna watafiti wanasema wakazi hao walikuwa Wairaki wa zamani.
Baadhi ya utamaduni
waliouacha Wairak hawa ni kulima kando ya mito maarufu kwa jina la finyungu, na
kutumia mawe ya kutoka mtoni kusagia nafaka.
Wahehe waliendeleza utamaduni huu na huita mawe hayo nunulilo.
Pia walikuwa na utamaduni wa kujenga majengo ya mviringo
kutumia mawe,mpaka miaka ya mwanzoni ya 60 kulikuwa na mabaki ya jengo la namna
hiyo kule Kiwiluka, ambalo lilikuja fumuliwa taratibu na watoto. Kule Engaruka,
Monduli kulikuwa na mabaki ya majengo ya aina hiyohiyo.
Katika bonde hilo la Lyambangali kulikuwa na masalia ya
majengo mengine, yaliyojengwa kwa matofali ya kuchomwa. Wahehe katika simulizi
zao za kale walisema waliojenga nyumba hizo walikuwa Waiyenzele,
Ugogoni kulikuwa na
masalia ya majengo kama hayo na Wagogo walisimulia kuwa wajenzi wa magofu yale
walikuwa Wamankala, lakini hakuna maelezo zaidi kuhusu watu hawa kuwa
Waiyenzele au Wamankala walikuwa wa aina gani , walitoka wapi, na walienda
wapi.
Watu wengine waliokuweko katika nchi hii walikuwa ni
Mbilikimo. Kuna hadithi za kale za Wahehe kuwa hawa Mbilikimo walikuwa hodari
kwa mishale, kwa vile walikuwa wafupi walikuwa wanawaona watu wengine mapema na
kupiga kelele ‘Ngulenge’ yaani
nimekwisha kulenga.
Kama mtu alimuona Mbilikimo kwanza alimwambia ,
Nguwene’ maana yake nimekuona, na hawa
mbilikimo, walikuwa wakiuliza umbonie kwi? Kwa sababu hiyo mpaka zama hizi
Mbilikimo au watu wafupi Uheheni, hujulikana kwa jina la utani, Mwanangulenge
au Wambonie kwi
Kundi jingine la watu waliokuweko katika uwanda huu wa
Wahehe kabla ya ujio wa Wahehe walikuwa Wahamya au kwa Kiingereza huitwa
Bushmen, hawa ni wafupi lakini si wafupi kama mbilikimo na pia huwa ni weupe
kiasi.
Hawa walifika mpaka sehemu za Manyoni na kuanza
kuchanganyika na wenyeji, wajukuu za Wahamya hawa waliobakia Uheheni huitwa kwa
mwidikiso wa Mkemwa na mwiko wao (msilo), ni nyama ya pundamilia.
Ukoo wa kina Mwisaka chanzo chao ni Wahamya hawa.
Kundi la mwisho ni Vahumma, Wahehe hutamka Vahumba, ni kundi
ambalo kwa Kiingereza hujulikana kama
Hamitic.
Hawa nao walienda kuweka maskani yao katika bonde la
Lyambangali .
Tuesday, July 26, 2022
NDALINYELE KUUTSUNGWA BE ABE
Ndalinyele Kuutsungwa - be abe
Ndililige tunutunu -be abeTwaanige datsudatsu - be abe
Nda kagombo ka Utsungwa - be abe
Wa wonige unegulile - be abe
Nge nige negule -be abe
Twitang'ana libohola -be abe
Likwanuka libohola -be abe
Wawonige upokapoke =be abe
Nge nige moka moke -be abe
Likwingila mugupango -be abe
Wawonige uhengahenge -be abe
Nge ninge nyenga nyenge - be abe
Ilihengo lyadumwike - be abe
Wawonige uponda ponde - be abe
Nge ninge monda monde - be abe
Avaponzi vasisile -be abe
Asige yukiwale - be abe
Ya kupondaga libume - be abe
kasimo dumu
Monday, July 25, 2022
TWIYENGELIGUTUGIMBI - KUKULEKU...simo 1
Twiyengeligu tugimbi - kukuleku
Na umuyangu kasogolo - kukuleku
Tukisindikila kwivaha - kukuleku
Vakutupela ligida - kukuleku
Tukima tukikanila - kukuleku
Vakatupela likolo -kukuleku
Tukwitumbulila katumbu - kukulekuTukyanikilia pi figa - kukuleku
Ikasi imbwa yi vaha - kukuleku
Kwe ihumile kwekwenula - kukuleku
Ve mbwa ve utegwe kiki - kukuleku
Ye negwe tengefiga - kukuleku
Wusu utengele ipa - kukuleku
Pagonile nyambuya - kukuleku
Nyambuya kidibwidibwi - kukuleku
Yakudibulagu utulenga -kukulele
Tulenga twa vanu vehe - kukulele
Kasimi dumu
KALIBUNI MULIBULOGU LYA KIHEHE
KUNA LIMJAMAA DE LIMBUSIGE ENE NDIWESA KUGITA MANYI IBLOGU YA KIHEHE, SWE NIGE SAWA, IBOLOGU IYI IPA. INO NDISUKU UMUSAADA ENE WINA IHADISI YA KIHEHE, APAMWI WINA KINU CHOCHOTE WISAKA KIWONEKANE MU BLOGU IYI, VE NZANDIKILE NEKE NDETELE MU WATSAP 0713274747.... ALE NYELA KINU IKI IPA TUVANGI IKASI