Pages

Sunday, July 31, 2022

UNAJUA KUWA ZAMANI MHEHE MWANAUME AKIFA ANAZIKWA NA MKEWE ALIYE HAI?


 

Kama nilivyoeleza katika makala zilizopita, wale  watu weupe waliowatimua Wategeta walikuwa pia wakifanya biashara ya kuuza watumwa. Koo nyingi za Kihehe hazikukubali kuuuzwa hivyo wengine waliona heri wauwawe, wengine waligoma kula hivyo kufa wakiwa katika masafara wa kuelekea pwani, na wengine walikimbia mbali kutoka maeneo yao ya asili.
Tuliona jinsi kabila la  Wanyakyusa lilivyopatikana kutokana na kusambaratika huko. Wagogo pia ni kabila lilitokana na fujo hizo. Koo mbalimbali za Wahehe walikimbilia kaskazini na kufika mpaka sehemu inaitwa Mkofa kando ya mto Lyambangali,  wakawa wanatafuta namna ya kuvuka kwenda upande wa pili, sehemu moja wakakuta gogo kubwa limeanguka na kulala juu ya mto na kutengeneza aina ya daraja, hivyo wakaweza kuvuka kumkimbia adui, kwa kukumbuka kuvuka huko, wahehe wale walijiita Vanyagogo, jina ambalo baadae likafupishwa kuwa Wagogo.
Wagogo wengi kwa kukumbuka walikotoka huwaita Wahehe wajomba zao. 
Kuna simulizi za kale kuwa Warangi walitokana na watu watu weupe waliohamia Uheheni  kutoka Usambara.
Wakati ule koo kadhaa zilizokuwa zikiishi karibu na bahari ya Hindi zilijikuta zikiwa na machotara wengi wa Kiarabu na baadae waKireno. Watu hawa weupe toka Usambara walikuja kuishi sehemu ya Ugunda iliyokuwa ikiitwa Ilamba na wengine kuhamia Usagala.
 Kuna Wasagala wa zamani walikuwa weupe na wanaume wakawa na nywele nyingi mikononi na kifuani na walikuja kuwa na muitiko au mwidikiso wa Mnyakami, inawezekana walikuwa na  uhusiano na Wakami wa Ulugulu. Hawa watu weupe walienea  sehemu nyingi za Uhehe, Ubena na Ukimbu.  Wale waliobaki Ugunda, Wahehe walianza kuwaita Valangi. Valangi  hawa na ndugu zao Wanyiramba walikuja kuhamia maeneo ilipo Singida sasa. Kuna wakati wajukuu wa Valangi hawa waliamua kurudi kwao Uheheni, lakini karibu na Dodoma wakakutana na ukoo wa Wadongwe waliokuwa chini ya Kiongozi wao Muyovela, vita kali ikaanza  wakashindwa na wakalazimika kukimbilia ilipo Kondoa sasa na huko wakaishi na kuongezeka na kuwa kabila kubwa.
Makundi mengine ya watu weupe  yalisonga mbele mpaka Ukimbu,  kundi jingine likahamia sehemu za Ilembula, kundi jingine likahamia kwa muda sehemu za Wasa, kisha kuelekea Malangali.
Kundi hili ndilo linalosemekana liliingiza kilimo cha kulima mahala kwenye majani kwa kugeuza udongo na kutengeneza matuta kwa kufukia majani. Majani yale yaliachwa kwa muda ili yaoze na kisha ndipo mbegu hupandwa.
Kilimo hiki kilileta mazao mengi, killimo hiki kiliitwa Malongo, na sehemu ile ya malangali ikaitwa Ilongo.  
Wahehe huita mavuno mengi kuwa ni Sanga. Katika sehemu hiyo ya Ilongo kukaweko na kundi fulani la wakulima waliokuwa hodari wa kulima malongo na hivyo kuwa wanapata mavuno mengi wakaanza kuitwa Vanyasanga, mafanikio ya Vanyasanga yakwaletea maadui na wakaamua kuhamia sehemu za Ukinga na Uwanji, na ndio chanzo cha koo za Sanga huko Ukinga na Uwanji.
Ukoo wa Kihaule pia husema walitokea Ilongo, na hata mwitiko wa binti wa kina Kihaule ni Nyamalongo. Wazee wa Upangwa husema kina Kihaule wa kwanza kuingia huko walikuwa weupe na walileta kilimo cha malongo, pia ndio waliokuja kusitisha mila ya kumzika mke akiwa mzima mzima kama mumewe amefariki, mila hii hata Wahehe awali  walikuwa nayo. 

No comments:

Post a Comment

STAT COUNTER