Pages

Showing posts with label Image. Show all posts
Showing posts with label Image. Show all posts

Tuesday, August 9, 2022

KABLA YA KUWA KABILA MOJA, UHEHE ILIKUWA NA VIKABILA MBALIMBALI KARIBU THELATHINI

 

Wahehe

Kabla ya Wahehe kuwa kabila moja kama linavyojulikana sasa kulikuwa na vikabila vidogovidogo karibu 30, na kila kimoja kikiwa chini ya ukoo kama ndio watawala. Tuanze na ukoo ulioitwa VaMudemu, .hawa walitawala katikati ya Ubena na Ulanga, maeneo kama  Ifwagi mpaka ilipo Malangali leo yalikuwa maeneo chini ya ya VaMudemu.  Ukoo huu unasemekana ulianzishwa na muwindaji  aliyeitwa Bugoma aliyetoka Ndweve iliyoko kwenye bonde la Ulanga. Mtiririko  wa watawala hao ulianza na Bugoma, akafuata Silonga, akafuata Nolelo, akafuata Mudemu, akaja Msambila, akafuata Mtamile na kumalizikia na Jumbe Hassan.
Kulikuwa na ukoo mwingione wenye jina la VaMudemu hawa ni wa Ndevelwa maeneo ya Isimani, hawa walikuwa ni ukoo tofauti na nilioutaja hapo awali.
Utawala mwingine Uheheni ulikuwa ni wa Ukalinga, huu ulikuweko kwenye milima ya Udzungwa. Kuna hadithi za mapokeo kuwa machifu hawa  wa Kalinga walitoka Unyakyusa, na ndio maana kuna Wanyakyusa wengi tu ni wa ukoo wa Mwakalinga, lakini pia kuna ile historia kuwa Wanyakyusa walitokana na ukoo wa Chusi  kama nilivyoeleza katika makala moja hapo nyuma.
Kuna akina Mwakalinga wengine wanasema chanzo cha ukoo wao ni Mufwimi Mwakalinga,  aliyefika Kisanga katika nchi ya Ukalinga na akampa mimba Sekikungile, na akakimbia na kumuacha binti huyo mja mzito. Sekikungile akamzaa Mupogole aliyekuja kutawala eneo la Ukalinga lililokuwa likikaliwa na Vadzungwa ambao hawakuwa na mtawala.
Mlolongo wa utawala huo ulikuwa hivi, kulikuwa na Mpogole aliemuoa Sekatefu, akafuata Lubida aliyemuoa Sepulamu, akaja  Mumehwa aliyeoa  Sekindole, akafuata Makanya aliyemuoa Semugele, akarithi Mugabe aliyemuoa  SeKindole, akarithi Mwanasindava aliyemuoa Semudalingwa, akafuatia Chotisamba aliyekuja kumzaa Hamisi aliyekuja kuwa sub chief wa mwisho  Ukalinga. Kuna kitu hapa cha kujihadhari, hadithi ya muwindaji kufika mahali  na kumpa mimba mtoto wa Chifu huwa inajirudia rudia katika simulizi nyingi za Uheheni, hivyo ni ya kuichukua kwa tahadhari kwa vile ni mapokeo. Lakini ukweli ni kuwa na kulikuwa na Wakalinga wengi katika eneo lililoitwa Ukalinga. Hii ilikuwa ni eneo mashariki mwa Mdabulo. Hivyo nyakati za mwanzo za utawala wa Muyugumba, Vakalinga nao walikuwa na utawala wao, na walikuwa wanaheshimika kiasi hata cha kufika Lugemba na kuoa akina Sekindole waliokuwa wa koo za kitawala.
Kulikuwa na kabila la Vategeta, hawa walikuwa na kiongozi aliyeitwa Nyembe au Nyembeke, Vategeta wanasemekana waliishi maeneo jirani na Ilula. Uzazi wao ni pamoja na wakina  Kihwaganise.

Ngoja nizitaje baadhi ya tawala ndogo ndogo na viongozi wao zilizokuweko kabla ya Uhehe kuwa moja;

 

1.       Igavilo, mtawala Kindole

 

2.       Savila mtawala Mandili

 

3.       Hafiwa mtawala Lyelu

 

4.       Nyandevelwa mtawala Mudemu

 

5.       Dongwe mtawala Mudung’u

 

6.       Nyimage mtawala Maginga

 

7.       Nyilambo mtawala Kitalika

 

8.       Nyilole mtawala Kihwaganise

 

9.       Tegeta mtawala Nyembe

 

10.   Fwagi mtawala Mudemu

 

11.   Ukalinga mtwala Kalinga

 

12.   Chalamila mtawala Chalamila

 

13.   Sagala mtawala Mukwando

 

14.   Sagala mtawala Mwigombe

 

15.   Nyaganilwa mtawala Mugovano

 

16.   Dzungwa mtawala Kahemela

 

17.   Dzungwa mtawala Njole

 

18.   Sagala mtawala Lwafu

 

19.   Sagala mtawala Mulandali

 

20.   Sagala mtawala Wutalo

 

21.   Dekwa mtawala Muhanga

 

22.   Dene mtawala Mulefi

 

23.   Nyamudenye mtawala  Mandongo

 

24.   Nyamugovelo (Sagala) mtawala Mutalula

 

25.   Nyang’uluhe mtawala Mududa

 

26.   Ilongo mtawala Mduda

 

27.   Ilongo mtawala Lukungu

 

28.   Kinamuyinga mtawala Muyinga


Sunday, August 7, 2022

MAELEZO YA ZIADA KUTOKA KWA MZEE MKOCHA KUHUSU MUFWIMI

 



Simulizi kuhusu Mufwimi ni simulizi nzuri na ina uhalisia fulani. Kwa mujibu wa akina Mwamuyinga wa Image, Avanyidaha wote walikuwa wawindaji; tofauti kubwa aliyoleta Mfwimi ilikuwa ushujaa wake wa kuua mnyama mkubwa, nyati, kwa mara ya kwanza na umaarufu wa Mfwimi wa pili, alikuja na chumvi, ambayo haikuwepo. Chumvi iliwawezesha jamii ile kula nyama nyingi. Na hasa ndiyo ilikuwa kivutio cha Mfwimi kwa Mwamduda na kwa muda mfupi watu hawa wakanawiri wakawa na nguvu. Hata huyu kijana aliyezaliwa na Se Mduda licha ya uwindaji, alikuwa mtundu na jeuri kupindukia.
Wakati wa utoto wangu mwanzoni mwa miaka ya 1950, kule kwetu Image kulikuwa na utaratibu wa kupimana nguvu kwa kupigana. Kila Kijiji kulikuwa na kijogoo wa ngumi, na kulikuwa na utaratibu wa kijogoo mmoja kutawala sehemu kubwa.
Wanaume walikuwa wanapigana bila kuwa wamegombana ila tu kuonyeshana ubabe. Mwamba mmoja alikuwa anasimama mbele ya watu kwenye mkusanyika hata kama ni kilabuni au hata kusanyiko la msibani, na kujitangaza kuwa anaeona kuwa ni kijogoo ajitokeze atetee heshima yake. Na kweli ilikuwa inatokea vurugu hapo mpaka kijogoo mmoja anapatikana.
Mimi nimeanza kwenda shule 1957, kijogoo wa Image wakati huo alikuwa Mwamadate. Akikasirika mishipa ya damu ya mikononi inatokeza mithili ya mkono wa mtoto mchanga. Ngumi yake ni kifo ikimpata mpinzani kichwani. Mwamba wa kujengea nyumba ya liking'a ya vyumba 3,  anatoka nao milimani amebeba kama unyasi wakati wenzie hata kuusimamisha huo mwamba, wanasaidiana watu kadhaa!
Kwa hiyo hata majeshi ya watu hawa walioshiba nyama, maziwa na ugali wa ulezi yalikuwa na afya kweli kweli. W
aandishi wengi wa historia ya Waafrika wanasahau kuelezea jinsi lishe bora ilivyowafanya watu wa zamani wawe wakakamavu walioweza kufanya mambo mengi ya ajabu.

STAT COUNTER