Pages

Thursday, September 20, 2012

KWA WALIOSOMA SHABAHA KATI YA 1971

Robert Nyato alijiunga na shule ya msingi ya Shabaha, ambayo awali ilikuwa ikiitwa Aga Khan Primary School. Jina la Shabaha lilitokana na kuwa, nyuma tu ya shule , pale mbele ya nyumba za Mzee Poyo palikuwa na sehemu ambayo askari wa FFU walikuwa wakitumia katika kujifunza kulenga shabaha, watoto waliokuweko wakati huo watakumbuka kuwa mara baada ya mazoezi ya shabaha watoto walikuwa wakienda kuokota maganda ya risasi yaliyotumika. Mkuu wa shule hii wakati huo alikuwa Mwalimu Chungu, Robert alikuwa na rafiki yake Evaristo Kimile. Walimu waliokuweko wakati huo walikuwa Mwalim Mama Mbaruku ambaye ndiye alikuwa mwalimu wa darasa la kwanza, Mwalimu Kitojo akiwa mwalimu wa nidhamu. Hatimae alifikia kuingia shule ya Highlands alipokutana na rula za mwalimu mkuu mwalim Sheikh, akisindikizwa na mwalimu Chalamila,Mwalimu Mwambeta,, Shawala, Mwal Mayagila, Mama Masima, Mwal Mpete, na Mwakalinga ilikuwa ni listi tosha ya kuhakikisha akina Mohamed Siaga, Ally Sareva, Maneno Ndanzi na Robert Kipandule Nyato wanasoma ipasavyo.....una kumbukumbu za enzi zako? zitume kwa sms 0713274747 au jkitime@gmail.com zitundikwe kwenye blog hii ASANDE

No comments:

Post a Comment

STAT COUNTER