Pages

Sunday, September 30, 2012

KIKAO CHA WANAKIHESA CHAFANA

Kikao cha wanaKihesa kilichofanyika KGB Hotel Jumapili hii tarehe 30 September, kilifana kwa ongezeko kubwa la washiriki wa kikao hicho. Pamoja na mengine, kwa sasa lengo kubwa ni kuwa na Tamasha la Wana Kihesa tarehe 2 Desemba 2012, ambalo limepangwa kuwepo katika eneo la Kijiji cha Makumbuso.  Baadhi ya wanaKihesa walioonekana katika kikao cha safari hii ni pamoja na Mikidadi Mwachang'a ambae alisema wazi na kwa uchungu kuwa alikuwa anaombea uwepo wa umoja wa namna hii miaka mingi. Mwana kihesa mwingine alikuwa ni mwana Kihesa maarufu Fredrick Mwakalebela ambae nae pia aliahidi kuwa bega kwa bega katika kufanikisha umoja huu. Fedha taslimu shilingi  Laki 6 na nusu zilichangwa na ahadi za milioni moja zilitolewa. Mkutano ujao utakuwa tarehe 14 Oktoba katika ukumbi huohuo wa KGB Hotel, Ubungo Riverside

No comments:

Post a Comment

STAT COUNTER