Pages

Sunday, April 11, 2010

Aga Khan 3

Niligusia hapo awali kuwa nilipoingia Form One nilikuta wanafunzi wengi kutoka Mwanza wakiwa Form Two, ni karibuni tu ndio nilikuja fahamu sababu. Usitishwaji wa darasa la nane ulianza kwa awamu tofauti katika Kanda mbalimbali, kuna kanda ambazo zilianza kufuta darasa la nane tangu 1965, wakati Kanda ambayo Iringa ipo walifuta darasa la saba 1967. Hivyo basi wale wanafunzi waliolazimika kuingia Form One kutoka mikoa ya kaskazini walipelekwa mikoa ya kusini kama Iringa ambako kulionekana kuna nafasi, tatizo ni kuwa nafasi hii haikupatikana kwa wanafunzi wa ziada waliomaliza darasa la saba na la nanewaliotoka kusini, hivyo wengi kukosa nafasi ya kuendelea iliyokuwa imechukuliwa 1966. Pamoja na kuonekana ni jambo la kawaida lakini matokeo ya nafsi hizo kukosekana kwa wanafunzi wa kusini yanaonekana mpaka leo.

2 comments:

  1. Kamwene kaka Kitime. Nilikuwa sikjui kama wewe ni school mate.

    ReplyDelete
  2. Unajua mimi nipo Lebanon kwasasa. Najisikia raha sana kusoma habari za nyumbani hasa kukaye kwiringa na shule niliyosoma.

    ReplyDelete

STAT COUNTER