Pages

Thursday, April 8, 2010

Aga Kha Secondary 1


Mwaka 1967 ndipo darasa la nane lilipofutwa Mkoani Iringa, hivyo waliokuwa std VIII walifanya mtihani na std VII tayari kwa pamoja kusubiri kuchaguliwa kuingia Form One. Kati ya wanafunzi wanane tuliochaguliwa kuingia sekondari, waswahili tulikuwa wawili, Mheshimiwa aliyekuwa Mbunge Kisyeri Chambiri na mimi. Wengine sita walikuwa wahindi. Na wote tukachaguliwa kuingia Aga Khan Secondary Iringa. Kuingia sekondari ni experience nyingine. Nilikutana na rafiki zangu niliyoachana nao Consolata, kama Emmanuel 'Katuluta', Chesus, Naboth, Nuhu, na hata wale waliotutangulia kama Gerald, John Mzungu, Kandoro, na wengine wengi. Siku ya kwanza nakumbuka kabisa tulipewa mafyekeo na kuanza kufyeka majani,kila mtu akijihisi kuwa katika hatua mpya ya maisha. Mwaka 1966 ulikuwa umeanzishwa mpango ambao uliweza kufuta kabisa ukabila, kwa kuchanganya watu toka mkoa mmoja kwenda mwingine hivyo form 2 tulioikuta ilikuwa na wanafunzi wengi sana kutoka Mwanza hususan Wasukuma. Mchanganyiko huu ulifanya maisha ya shule ile kuwa na kumbukumbu nyingi sana za furaha. Rafiki yangu Kisyeri ambaye alikuwa na bongo inacheka sana hasa kwenye mahesabu aliamua kuhamia shule ya Ufundi Ifunda, mwenyewe akiwa na picha kamili kuwa anataka kuwa engineer. Nakumbuka barua zake za kwanza kwangu akiniandikia wanaproject ya kutengeneza Hoovercraft. Hiki ni chombo kinachoweza kutembea hewani majini na kwenye nchi kavu. Nasi tukaanza maisha ya form one tukiwa na waalimu wa Kimarekani waliokuwepo kutokana na mpango wa Peace Corps. Kasheshe ndipo lilipoanza, kufundishwa Kiingereza na Mmarekani, anamaliza kipindi hata akiwauliza 'Did ya understand?' Hamjui anasema nini, wala alikuwa anasema nini kipindi kizima. Maliwato

No comments:

Post a Comment

STAT COUNTER