Pages

Showing posts with label Fort Jesus. Show all posts
Showing posts with label Fort Jesus. Show all posts

Monday, August 1, 2022

JE UNAJUA MWITIKO AU MWIDIKISO WA MGONANZI ULITOKA WAPI? SOMA HAPA

WAZEE  wa zamani wa Kisambaa walikuwa wakihadithia kuwa kuna wakati kundi kubwa la Wahumba lilipita nchini kwao likielekea Kusini, ilikuwa ni wakati Waarabu wa Oman chini ya Mfalme wao Said Bin Sultan walipokuwa wakiwashambulia Wareno katika ngome  yao  Fort Jesus kule Mombasa. Kwa tarehe hizo ina maana Wahumba hao walipita Usambaa kati ya tarehe 13 March 1696 na 13 March1698.  Wahumba hao walikuwa wakiongozwa na Wahabeshi.  Wahumba hawa walikuwaa wametoboa masikio yao na kuyarefusha hadi kufikia karibu na mabega na hivyo masikio yalifanana na aina ya pembe za  ng’ombe ambazo hupinda na  kuangalia chini, pembe za aina hiyo hiyo huitwa Ngologo, hivyo Vahumba hawa walipoingia Uheheni walikuja julikana kama  Vanyangologo.
Vahumba hawa waliingia Uheheni kupitia Wota kisha wakavuka  Lyambangali na kuingia Ugunda. Kama nilivyokuhadithia katika masimulizi huko nyuma, Ugunda ilikaliwa na watu weupe ambao wenyeji waliwaita Valangi.
Wahumba hawa waliwashambulia Valangi na kukawa na mapigano makali watu wengi pande zote wakapoteza maisha na Valangi wakalazimika kukimbia na ndipo wakahamia Singida kama nilivyokuhadithia hapo awali.
Pale Ugunda kulitapakaa sime za Vahumba waliouwawa, na kwa kuwa wahehe huita sime Mage, mahala pale pakaitwa Image mpaka hivi leo.
Vanyangologo waliendelea na safari yao ya kusaka watu weupe huku wakiacha ndugu zao wengine kuwaangalia majeruhi pale Image. Safari hiyo ya kuwaska na kuwauwa watu weupe iliendelea mpaka Ilongo, Ubena, na hata Ukimbu.
Kitu cha ajabu ni kuwa Vahumba hawa hawakushughulika na Vakilwa, hivyo Vakilwa walikuja kuanza kutawala sehemu nyingi ambazo hawakuguswa.
Wale Vanyangologo waliobaki Image walianza mahusiano na wanawake wa Usagala, Hivyo katika sehemu za Image na Ilole kukawa na koo za wahehe ambao wanafanana na Wamasai kwa umbo, na sura zao za kuchongoka.
Wengi hukataa kuwa asili ya kizazi chao ni  Vahumba lakini wanadai asili yao ni Hamitic. Lakini Humma maana yake ni Hamitic. Akina Ngimba wa Ilole asili yao ni Vahumba. Itakumbukwa kuwa  mama mzazi wa Mutwa Mkwava alikuwa Sengimba.
Ukoo wa akina Sambala asili yao ni Wahamitic, hata mwitiko au mwidikiso wao ni Mugonanzi , maana yake mwenye kulala sehemu mbalimbali au mhamaji, kwa Kiingereza tungesema nomad na hiyo ndiyo ilikuwa sifa ya Vahuma.
Wale wasagala weupe hawakukwepa kusakwa na Wahumba, wengine wao walikimbilia Wota kwa kuvuka Lyambangali,hawa wakaja kujiita  Mlowoka. Kuna walowoka wengine walikuja kurudi Uheheni  kama ukoo wa Fivawo na Makombe wa Tanangozi na Iwawa. Mliotajwa mnasemaje?

 

 

 

 


STAT COUNTER