Pages

Sunday, December 2, 2012

MATUKIO KIHESA DAY 1



Mkunungu










Baada ya matayarisho ya siku ya Wanakihesa kwa miezi kadhaa , hatimae ndoto ya Wanakihesa ilitimia kwa siku hiyo kuweko na mamia ya wanaKihesa na wanaIringa kwa ujumla kujitokeza katika siku hii iliyojaa furaha, na kumbukumbu nyingi. Kama ilivyokuwa imepangwa katika vikao vya awali siku ya Wanakihesa ilikuwa ni siku ya wahusika kuonyesha shughuli zao mbalimbali katika siku hii. Hivyo basi wapishi walipika chakula na kuuza, wabunifu walileta vifaa vyao zikiwemo nguo na mapambo ya asili, watengenezaji wa sabuni walileta mali zao, kulikuweko na walioleta vyakula kama bagia za Iringa ambazo ziliisha mapema sana kama ilivyoisha mikusu na matundadamu, na mkunungu. Picha zifuatazo zilionyesha kazi mbalimbali za wajasilia mali wa Kihesa wakiwemo, book publishers waliokuja kuonyesha vitabu vya aina mbalimbali.

Sunday, November 18, 2012

WANAKIHESA WACHANGA ZAIDI YA MILIONI MBILI

Kikao cha matayarisho ya siku ya Wanakihesa 2/12/2012, inayotegemewa kufanyika Makumbusho Dar es Salaam kimekuwa cha mafanikio makubwa kwa wajumbe kuwa wengi zaidi, wajumbe wamezidi kufanikisha michango yao,na kuwa mpaka sasa zimekusanywa zaidi ya shilingi milioni mbili na nusu. Leo tena  kikao kilichangamka sana kikiwa na wajumbe wengi zaidi akiwemo Brown Mbigili, ambaye aliburudisha kikao kwa kutukumbusha Rais wa Kihesa…Mtambule marehemu Mzee Mbigili. Picha za kikao







































STAT COUNTER