Mkunungu |
Baada ya matayarisho ya siku ya Wanakihesa kwa miezi kadhaa , hatimae ndoto ya Wanakihesa
ilitimia kwa siku hiyo kuweko na mamia ya wanaKihesa na wanaIringa kwa ujumla
kujitokeza katika siku hii iliyojaa furaha, na kumbukumbu nyingi. Kama ilivyokuwa
imepangwa katika vikao vya awali siku ya Wanakihesa ilikuwa ni siku ya wahusika
kuonyesha shughuli zao mbalimbali katika siku hii. Hivyo basi wapishi walipika
chakula na kuuza, wabunifu walileta vifaa vyao zikiwemo nguo na mapambo ya
asili, watengenezaji wa sabuni walileta mali zao, kulikuweko na walioleta
vyakula kama bagia za Iringa ambazo ziliisha mapema sana kama ilivyoisha mikusu
na matundadamu, na mkunungu. Picha zifuatazo zilionyesha kazi mbalimbali za
wajasilia mali wa Kihesa wakiwemo, book publishers waliokuja kuonyesha vitabu
vya aina mbalimbali.