Pages

Friday, October 5, 2012

ENDELEA KUIJUA HISTORIA YA KIHESA

 WASIFU WA WAZEE WAANZILISHI WA KIHESA

 (1) MZEE JUMBE OMARY  
  Huyu mzee makazi yake ya mwanzo yalikuwa Kigonzile, baadae aliamia Kihesa karibu na mlima lilipo  kanisa la Kilutheli la Kihesa. alichaguliwa kuwa JUMBE,
Kazi yake aliamua kesi mbalimbali na kuwahamisha watu kuja eneo ilipo Kihesa kutoka  milimani, kwa mfano mlima Mafifi.
Kesi zilizo mshinda alizipeleka Kalenga wakati huo ndiko kulikwepo mahakama ya mwanzo. Mwandishi wa habari hii alimuona Mzee JUMBE OMARY mara ya mwisho mwishoni mwa miaka ya 1970. Alikuwa na ngeu usoni ambayo inasemekana  aliwahi kupigana na simba.

(2) AZIZA SEMGENI
 
 Bibi huyu ni mmoja wa waanzilishi wa Kihesa, yeye alikuwa anatibu kwa miti shamba, Eneo lake ndipo palipo jegwa shule ya msingi Kihesa. Wajukuu wa Bibi Aziza ni Mzee Jonas Mgeni ( Baba Zacho) Mzee Lwinusu Mgeni (Baba Riziki)

(3) SEMTEMA KUUKINGA
Mama huyu wa kabila la Kikinga aiifariki miaka michache aliopita ni mmoja wa waanzilishi wa Kihesa na alikuwa anamiliki eneo ambalo mpaka leo maarufu kwa jina la SEMTEMA  karibu kabisa na Chuo Kikuu cha Tumaini

(4) SALUMU SOSOVELE
Huyu mzee kwa waliobahatika kumuona alikuwa pandikizi la mtu. mwenye kuongea kwa tabasamu. Baba yake mzazi ndie aliyemiliki eneo kilipo jegwa Chuo Cha Elimu Kleruu.Na kaburi la baba wa Salum lipo jirani na Kanisa Katoliki Kihesa.

Wednesday, October 3, 2012

WAZEE MAARUFU WALIOIJENGA KIHESA




-->
  1. MZEE JUMBE OMARY
  2. MZEE LOTTI LUPEMBE
  3. MZEE ZABRON KIPANDULE MWANYATO
  4. MZEE PHOLIPO SAWANI
  5. MZEE RUBEN NYARUSI
  6. MZEE ANDREW MKOCHA
  7. MZEE METUSALA SINZIA MWAMOTTO
  8. MZEE NIKOLAI CHAWE
  9. MZEE PESAMBILI RAIS
  10. MZEE JUMANNE MWANDAMIZI
  11. MZEE JIMMY MWAMBAGO
  12. MZEE CAPRO MAHANJAM MDEGELA
  13. MZEE JOHN MAUYA
  14. MZEE FEDRICK KIHADE
  15. MZEE SHEM MAINGARA
  16. MZEE VICENT MSEMWA MFARANYAKI
  17. MZEE LUBAFU LWASOMBA
  18. MZEE ELEUTEL KIMILIKE
  19. MZEE RUPI SABA MKUSA
  20. MZEE GARUS KING'UNZA
  21. MZEE GARUS MWANYAKUNGA
  22. MZEE JAMES CHOMI
  23. MZEE WILLIAM MNG'ONG'O
  24. MZEE MATHAYO MNG'ONG'O
  25. MZEE METUSALA MNG'ONG'O
  26. MZEE PETER MSILU
  27. MZEE EDWARD MMASI
  28. MZEE GEORGE SAWALA
  29. MZEE LUCAS MKUSA
  30. MZEE MUSSA MWACHANG'A
  31. MZEE AUGUSTINO MWACHANG'A
  32. MZEE EMMANUEL MWACHANG'A
  33. MZEE MARTIN MLOWE
  34. MZEE JOHN NZALI BALANCE
  35. MZEE MKINGA SAFI MBILINYI
  36. MZEE AMOSI MPOGOLE
  37. MZEE SAID KITENGE
  38. SHEKHE MDOKA MAULID
  39. SHEKHE SAID KALELA
  40. SHEKHE SAID WANGUVU
  41. MAMA DIANA MAGRETH
  42. MZEE MPOGOLE (BABA SAREHE)
  43. MZEE ALEX SANGA
  44. MZEE ISAYA KAGAHE
  45. MZEE SAMSON NYATO
  46. MZEE SAMWEL KINYUNYU
  47. MZEE MALIO  MSILU
  48. MZEE HAMISI KINGENG'ENA
  49. MZEE NGAIRO( BABA STIVIN)
  50. MZEE KUDINGWA MAPUNDA
  51. MZEE FRANSIS KITIME
  52. MZEE LAMEKI TUMBUKA
  53. MZEE IBRAHIM MWIBARAMA
  54. MZEE KALYIEMBE ( BABA ANYWELWISE)
  55. MZEE SIXMUND MOLAMOLA
  56. MZEE JOSEPH KASUMRI SANGA
  57. MZEE  MKULU EZEKIA
  58. MZEE  CHODOTA (BABA ELIABI)
  59. MZEE MTEVELA (BABA FOIDA)
  60. MZEE OBADIA NGOGO
  61. MZEE PETER NGWIVAHA
  62. MZEE EDWARD MAKWETA
  63. MZEE ADAMU KAPUNGU
  64. MZEE ELIEZA MNG'ONG'O
  65. MZEE EDSON MWAMWANI
  66. MZEE JOHN LUSUNDE
  67. MZEE ZABRON KINYAMAGOHA
  68. MZEE EPHRANI KILATU
  69. MZEE SALUM NYENZI
  70. MZEE ADAM SAJIO KADUMA
  71. MZEE JONASI MGENI
  72. MZEE ZAKARIA CHUWA
  73. MZEE MAIGE MACHIBYA
  74. MZEE KUFAKUNOGA MAHAMODU
  75. MZEE PETER LUPEMBE
  76. MZEE LINGWENDU SANGA
  77. MZEE JOHN KANYWENDA 
  78. MZEE MARTINE MWAMBILINGE
  79. MZEE AMRAN MDEMU
  80. MZEE HENRY NYANYEMBE
  81. MZEE JOHN LUHANGA
  82. ZABRONI LUVINGA
  83. MZEE ALI MDUBA
  84. MZEE MARKO MFUGALE
  85. MZEE ALFREDY MBATA
  86. MZEE JOHN GILIKI
  87. MZEE JOHN EJO
  88. MZEE GALAHENGA BEATUSI
  89. MZEE MDENDEMI
  90. MZEE MWANYWAEGE
  91. MZEE DANIEL LUGENGE
  92. MZEE KIDUNU
  93. MZEE MNG'ONGO'
  94. MZEE MBILINYI
  95. MZEE MWANANGUNULE
  96. MZEE KANDANDA
  97. MZEE TITIKOO
  98. MZEE SALUM MDEGIPARA
  99. MZEE FUNGO
  100. MZEE MGOMBELE
  101. MZEE NZELU
  102. MZEE KIDULILE
  103. MZEE MBIFILE
  104. MZEE ELIAS SANGA
  105. MZEE NGWALE
  106. MZEE  MARTIN KIDUKO
  107. MZEE KIWELE
  108. MZEE MWITA
  109. MAMA GIFT
  110.  MZEE NGALAWA (BABA MWAMBA)
  111. MZEE DICKS DISUZA
  112. MZEE MAGAVA
  113. MZEE FARAHANI
  114. MZEE BENARD MBIGILI
  115. MZEE POYO
  116. MZEE MNYAMWANI
  117. MZEE KAPANDE
  118. MZEE MWALIWELO
  119. MZEE MALILA
  120. MZEE CHENGULA
  121. MZEE FURAHISHA
  122. MZEE  WILILO (BABA ROBERT)
  123. MZEE MASENYA
  124. MZEE BABA HILDA
  125. MZEE MASHAKA WILLBAKI
  126. MZEE KIKOSI JUMA MASOUD
  127. MZEE COSMAS MDESA
  128. MZEE MLIMBILA
  129. MZEE MBOMBWE
  130. MZEE SOSTEN KYANDO
  131. MZEE NDITI 
  132. MZEE BABA MAYASA
  133. MZEE WEEK END
  134. MZEE LUGENGE
  135. MZEE LUGALA
  136. MZEE MWANG'INGO
  137. MZEE ODO
  138. MZEE RUNYASI
  139. MZEE SEKAHANGA
  140. MZEE MFIKWA
  141. MZEE AMBROS MWANGWADA
  142. MZEE KIWONAOMELA
  143. MAMA SAMAMBA
  144. MZEE LUCHABIKO KAPUGI
  145. MCHUGAJI CHUSI
  146.  MZEE MACHILINA
  147. MAMA SEMPOGOLE
  148. MAMA GEORGE KUMBEMBA  MWAKIMBENGONDO MGODAGWIVAHA MUNYIDUNDA
  149. MZEE SAMUEL BWANANGONDO M.M MWAKIMBE
                                                         
                               
NB: KUNA WAZEE WASIOPUNGUA 200 WALIO IJENGA KIHESA TUTAENDELEE KUSAIDIANA KUWAKUMBUKA KAMA MAJINA YAO HAYAPO HAPA
                                    KATIKA MAANDALIZI YA SIKU YA WANA KIHESA TUTAKUWA TUNAWACHAMBUA WASIFU WA WAZEE HAWA.
                                IMETAYARISHWA NA ROBERT MWANYATO: MRATIBU WA TAMASHA LA WANA KIHESA

Sunday, September 30, 2012

KIKAO CHA WANAKIHESA CHAFANA

Kikao cha wanaKihesa kilichofanyika KGB Hotel Jumapili hii tarehe 30 September, kilifana kwa ongezeko kubwa la washiriki wa kikao hicho. Pamoja na mengine, kwa sasa lengo kubwa ni kuwa na Tamasha la Wana Kihesa tarehe 2 Desemba 2012, ambalo limepangwa kuwepo katika eneo la Kijiji cha Makumbuso.  Baadhi ya wanaKihesa walioonekana katika kikao cha safari hii ni pamoja na Mikidadi Mwachang'a ambae alisema wazi na kwa uchungu kuwa alikuwa anaombea uwepo wa umoja wa namna hii miaka mingi. Mwana kihesa mwingine alikuwa ni mwana Kihesa maarufu Fredrick Mwakalebela ambae nae pia aliahidi kuwa bega kwa bega katika kufanikisha umoja huu. Fedha taslimu shilingi  Laki 6 na nusu zilichangwa na ahadi za milioni moja zilitolewa. Mkutano ujao utakuwa tarehe 14 Oktoba katika ukumbi huohuo wa KGB Hotel, Ubungo Riverside

Thursday, September 20, 2012

KWA WALIOSOMA SHABAHA KATI YA 1971

Robert Nyato alijiunga na shule ya msingi ya Shabaha, ambayo awali ilikuwa ikiitwa Aga Khan Primary School. Jina la Shabaha lilitokana na kuwa, nyuma tu ya shule , pale mbele ya nyumba za Mzee Poyo palikuwa na sehemu ambayo askari wa FFU walikuwa wakitumia katika kujifunza kulenga shabaha, watoto waliokuweko wakati huo watakumbuka kuwa mara baada ya mazoezi ya shabaha watoto walikuwa wakienda kuokota maganda ya risasi yaliyotumika. Mkuu wa shule hii wakati huo alikuwa Mwalimu Chungu, Robert alikuwa na rafiki yake Evaristo Kimile. Walimu waliokuweko wakati huo walikuwa Mwalim Mama Mbaruku ambaye ndiye alikuwa mwalimu wa darasa la kwanza, Mwalimu Kitojo akiwa mwalimu wa nidhamu. Hatimae alifikia kuingia shule ya Highlands alipokutana na rula za mwalimu mkuu mwalim Sheikh, akisindikizwa na mwalimu Chalamila,Mwalimu Mwambeta,, Shawala, Mwal Mayagila, Mama Masima, Mwal Mpete, na Mwakalinga ilikuwa ni listi tosha ya kuhakikisha akina Mohamed Siaga, Ally Sareva, Maneno Ndanzi na Robert Kipandule Nyato wanasoma ipasavyo.....una kumbukumbu za enzi zako? zitume kwa sms 0713274747 au jkitime@gmail.com zitundikwe kwenye blog hii ASANDE

MKUTANO WA WANAKIHESA 30 SEPTEMBER 2012 KGB HOTEL

 Mratibu wa WanaKihesa Robert Kipandule Mwanyato anawaomba wana Kihesa kuhudhuria kwa wingi kikao muhimu tarehe 30 September 2012, katika ukumbi wa Hoteli ya KGB iliyopo Riverside Ubungo. Pia angependa kuwataarifu wote kuwa viongozi wa liochaguliwa katika kikao cha terehe 9 September 2012 ni kama wafuatao;
Mlezi-Sethi Motto
Mwenyekiti-Nordrick J Mbago
Makamu Mwenyekiti- Richard Mkocha
Katibu -Bright Robert Nyato
Katibu Msaidizi-Devota Peter Msilu
Mtunza Hazina Alfred Mlowe
TUNAOMBA TUHUDHIRIE MKUTANO HUO KWA WINGI

Sunday, September 16, 2012

WANAKIHESA WA DAR ES SALAAM, WAKUTANA KUPANGA MAMBO YAO

Mkutano wa pili WanaKihesa ulifanyika leo katika hotel ya KBG maeneo ya Riverside Ubungo. Nia ya mkusanyiko huu ni kuangalia namna ya WanaKihesa kuweza kukutana na kushirikiana katika mambo yao ya pamoja. Tarehe 2 Dec 2012 ni siku ambayo imekubalika kuwa siku ya WanaKihesa, hivyo kutakuwa na shughulimbalimbali zitakazofanyika siku hiyoikiwemo chakula cha pamoja vinywaji, na michezo mbalimbali ikiwemo muziki wa bendi hasa Tancut.MKutano ujao tarehe 30 September 2012












STAT COUNTER